005-Maswali 200 Na Majibu Ya 'Aqiydah: Wakati Gani 'Amali Inakuwa 'Ibaadah?

 

    200 سُؤالٌ وَ جَوَابٌ فِي الْعَقِيدَة

Maswali 200 Na Majibu Ya ‘Aqiydah

 

لِلشَّيخ حافِظ بن أحْمَد الحَكمَيّ 

Shaykh Haafidhw Bin Ahmad Al-Hakamiyy (رحمه الله)  

Imefasiriwa na:  Alhidaaya.com

 

005-Wakati Gani 'Amali Inakuwa 'Ibaadah?

 

 

 

Swali:

 

متى يكون العمل عبادة؟

Wakati gani ‘amali (matendo) inakuwa ‘Ibaadah?

 

 

Jibu:

 

ج: إذا كمل فيه شيئان وهما كمال الحب مع كمال الذل قال الله تعالى (والذين آمنوا أشد حبا لله) وقال تعالى  (إن الذين هم من خشية ربهم مشفقون) وقد جمع الله تعالى بين ذلك في قوله   (إنهم كانوا يسارعون في الخيرات ويدعوننا رغبا ورهبا وكانوا لنا خاشعين)

 

Matendo yanakuwa Ibaadah yanapotimia ndani yake mambo mawili nayo ni: Ukamilifu wa upendo pamoja na ukamilifu wa unyenyekevu.

 

Allaah (سبحانه وتعالى) Anasema:

 وَالَّذِينَ آمَنُوا أَشَدُّ حُبًّا لِّلَّـهِ  

Na wale walioamini wana mapenzi zaidi kwa Allaah [Al-Baqarah: 165]

 

Anasema pia Allaah (سبحانه وتعالى):

 

إِنَّ الَّذِينَ هُم مِّنْ خَشْيَةِ رَبِّهِم مُّشْفِقُونَ ﴿٥٧﴾

Hakika wale ambao kwa kumuogopa Rabb wao, bado ni wenye kuchelea (Adhabu Yake). [Al-Muuminuwn: 57]

 

Na mambo hayo Allaah (سبحانه وتعالى) Ameyakusanya katika Aayah kwa kusema:

إِنَّهُمْ كَانُوا يُسَارِعُونَ فِي الْخَيْرَاتِ وَيَدْعُونَنَا رَغَبًا وَرَهَبًا ۖ وَكَانُوا لَنَا خَاشِعِينَ ﴿٩٠﴾

Hakika wao walikuwa wakikimbilia katika mambo ya khayr na wakituomba kwa raghba na khofu, na walikuwa wenye kutunyenyekea. [Al-Anbiyaa: 90]

 

  

 

Share