01-Wewe Pekee Tunakuabudu: Maana Ya Du'aa Kilugha Na Ki-Iswtwilaah

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada.

 

01-Maana Ya Du’aa Kilugha Na Ki-Iswtwilaah

 

 

Maana Ya Du’aa Kilugha:

 

 

Neno du’aa asili yake ni kuita kwa sauti, mfano kumwita mtu, au kusema ameitwa ameitikia, au kuita wito fulani n.k. Mifano katika Kauli za Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

قَالَ رَبِّ السِّجْنُ أَحَبُّ إِلَيَّ مِمَّا يَدْعُونَنِي إِلَيْهِ ۖ وَإِلَّا تَصْرِفْ عَنِّي كَيْدَهُنَّ أَصْبُ إِلَيْهِنَّ وَأَكُن مِّنَ الْجَاهِلِينَ﴿٣٣﴾

(Yuwsuf) Akasema: “Ee Rabb wangu! Nastahabu zaidi jela kuliko yale wanayoniitia. Na Usiponiepusha na vitimbi vyao nitaelemea kwao na nitakuwa miongoni mwa majahili.” [Yuwsuf: 33]

إِنَّ الشَّيْطَانَ لَكُمْ عَدُوٌّ فَاتَّخِذُوهُ عَدُوًّا ۚ إِنَّمَا يَدْعُو حِزْبَهُ لِيَكُونُوا مِنْ أَصْحَابِ السَّعِيرِ ﴿٦﴾

Hakika shaytwaan kwenu ni adui, basi mfanyeni kuwa ni adui. Hakika anaitia kikosi chake ili wawe miongoni mwa watu wa moto uliowashwa vikali mno. [Faatwir: 6] 

 

يَوْمَ يَدْعُوكُمْ فَتَسْتَجِيبُونَ بِحَمْدِهِ وَتَظُنُّونَ إِن لَّبِثْتُمْ إِلَّا قَلِيلًا ﴿٥٢﴾

 “Siku Atakayokuiteni, basi mtamuitika kwa Himidi Zake; na mtadhania kuwa hamkubakia (duniani) isipokuwa kidogo tu.” [Al-Israa: 52]

 

فَجَاءَتْهُ إِحْدَاهُمَا تَمْشِي عَلَى اسْتِحْيَاءٍ قَالَتْ إِنَّ أَبِي يَدْعُوكَ لِيَجْزِيَكَ أَجْرَ مَا سَقَيْتَ لَنَا ۚ فَلَمَّا جَاءَهُ وَقَصَّ عَلَيْهِ الْقَصَصَ قَالَ لَا تَخَفْ ۖ نَجَوْتَ مِنَ الْقَوْمِ الظَّالِمِينَ ﴿٢٥﴾

Basi akamjia mmoja kati ya wanawake wawili akitembea kwa kuona hayaa; akasema: “Baba yangu anakwita ili akulipe ujira wa kutunyweshea.” Basi alipomfikia na akamsimulia visa vyake; alisema: “Usikhofu, umeokoka na watu madhalimu.” [Al-Qaswasw: 25]

 

 

Maana Ya Du’aa ki Iswtwilaah:

 

Ni kitendo cha ‘ibaadah  kwa kumkabili Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kumuomba jambo kwa kuyakinisha kwamba Yeye Pekee Ndiye Anaepokea maombi kisha Ayaitikie kama Anavyosema (Subhaanahu wa Ta’aalaa):

 

 

وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌ ۖ أُجِيبُ دَعْوَةَ الدَّاعِ إِذَا دَعَانِ ۖ فَلْيَسْتَجِيبُوا لِي وَلْيُؤْمِنُوا بِي لَعَلَّهُمْ يَرْشُدُونَ﴿١٨٦﴾

Na watakapokuuliza waja Wangu kuhusu Mimi, basi Mimi ni Niko karibu (kwa ujuzi); Naitikia du’aa ya muombaji anaponiomba. Basi waniitikie Mimi na waniamini Mimi, wapate kuongoka. [Al-Baqarah: 186]

 

Mifano michache kutoka katika Qur-aan:

 

هُنَالِكَ دَعَا زَكَرِيَّا رَبَّهُ ۖ قَالَ رَبِّ هَبْ لِي مِن لَّدُنكَ ذُرِّيَّةً طَيِّبَةً ۖ إِنَّكَ سَمِيعُ الدُّعَاءِ ﴿٣٨﴾

Hapo hapo Zakariyyaa akamwomba Rabb wake, akasema: “Rabb wangu Nitunukie kutoka Kwako kizazi chema hakika Wewe ni Mwenye kusikia du’aa yangu.” [Aal-‘Imraan: 38]

 

 

رَبَّنَا آتِنَا فِي الدُّنْيَا وَمَا لَهُ فِي الْآخِرَةِ مِنْ خَلَاقٍ ﴿٢٠٠﴾

“Rabb wetu Tupe katika dunia;” naye katika Aakhirah hana sehemu yoyote. [Al-Baqarah: 38]

 

 رَّبِّ زِدْنِي عِلْمًا ﴿١١٤﴾

“Rabb wangu! Nizidishie elimu.” [Twaahaa: 114]

 

 Mifano katika Sunnah:

 

 

اللَّهُمَّ إِنِّي ظَلَمْتُ نَفْسِي ظُلْمًا كَثِيرًا وَلاَ يَغْفِرُ الذُّنُوبَ إِلاَّ أَنْتَ فَاغْفِرْ لِي مَغْفِرَةً مِنْ عِنْدِكَ وَارْحَمْنِي إِنَّك أَنْتَ الْغَفُورُ الرَّحِيمُ

Ee Allaah, hakika nimedhulumu nafsi yangu dhuluma nyingi wala hakuna wa kughufuria madhambi isipokuwa Wewe, basi Nighufurie maghfirah kutoka Kwako na Nirehemu, hakika Wewe ni Mwingi wa Kughufuria Mwenye Kurehemu daima [Al-Bukhaariy, Muslim, At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Ibn Maajah, Ahmad]

 

  اَللَّهُمَّ يَا مُقَلِّبَ الْقُلُوبِ ثَبِّتْ قَلْبِي عَلَى دِينِك

((Ee Mwenye kupindua nyoyo, Thibitisha moyo wangu katika Dini Yako [At-Tirmidhiy, Ibn Maajah, Ahmad, Al-Haakim  na Taz Swahiyh Al-Jaami’ 7987]

 

اللَّهُمَّ إِنِّي أَسْأَلُكَ الْجَنَّةَ وَأَسْتَجِيرُ بِكَ مِنَ النَّارِ

Ee Allaah, hakika mimi nakuomba Pepo na najilinda Kwako dhidi ya Moto [At-Tirmidhiy, An-Nasaaiy, Ibn Maajah – Swahiyh At-Tirmidhiy (2/319]

 

  اللّهُـمَّ أَعِـنِّي عَلـى ذِكْـرِكَ وَشُكْـرِك ، وَحُسْـنِ عِبـادَتِـك

Ee Allaah nisaidie juu Kukudhukuru, na kukushukuru na kukuabudu kwa uzuri utakikanao. 

[Abu Daawuwd, An-Nasaaiy]

 

 

Share