Je, Inafaa Kuibia Serikali Mita Za Taa?
SWALI
assalaam alaikum nashkuru sanaa kwa kunijibu maswali yangu mengi alla akulipenl ila nna tatizo jengine mimi kama mnavojua huku kwetu zanzibar matumizi ya umeme ni madogo kwenye nyumba zetu lakini hubambikiziwa bili kubwaa pengine kwa mwezi utalipa hata sh 30000 sasakuna fundi ataibana mita nitalipa sh 7000tu kwa mwezi jee mashekh wetu kisheria inafaa?
JIBU:
BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu wa Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa aalihi wa
Tunashukuru kuona kwamba ndugu zetu wako katika khofu ya kujiepusha na maovu na kuchuma dhambi na hivyo ndivyo anavyotakiwa Muislamu awe kila anapokosa ajirudi.
Lakini kuna dhambi ambazo hugeuka kuwa ni dhulma nazo ni baina ya mja na Mola wake
عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال (( أتدرون ما المفلس)) قالوا المفلس فينا يا رسول الله من لا درهم له ولا متاع قال رسول الله صلى الله عليه وسلم )) المفلس من أمتي من يأتي يوم القيامة بصلاته وصيامه وزكاته ويأتي قد شتم هذا وقذف هذا وأكل مال هذا وسفك دم هذا وضرب هذا فيقعد فيقتص هذا من حسناته وهذا من حسناته فإن فنيت حسناته قبل أن يقتص ما عليه من الخطايا أخذ من خطاياهم فطرح عليه ثم طرح في النار)) ألترمذي
Imetoka kwa Abu Hurayrah رضي الله عنه kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema: ((Mnamjua nani aliyefilisika)) Wakasema (Maswahaba): Aliyefilisika ni yule miongoni mwetu asiyekuwa na dirham au
Kitendo hicho cha kubana mita za umeme wa serikali ili itembee polepole na uweze kulipa gharama ndogo, ni kitendo cha wizi na Allaah سبحانه وتعالى Amelikataza jambo hili kwa makatazo makali kabisa hata Ametoa hukmu yake kuwa ni kukatwa mkono:
Anasema Allaah سبحانه وتعالى
وَالسَّارِقُ وَالسَّارِقَةُ فَاقْطَعُواْ أَيْدِيَهُمَا جَزَاء بِمَا كَسَبَا نَكَالاً مِّنَ اللّهِ وَاللّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ
((Na mwizi mwanamume na mwizi mwanamke, ikateni mikono yao, hayo ni malipo ya waliyoyachuma, ndiyo adhabu ya mfano itokayo kwa Mwenyezi Mungu. Na Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu na Mwenye hikima)) [Al Maaidah: 38]
Nayo pia huwa ni dhulma pindi hatorudisha mtu haki hiyo aliyochukua. Na inabidi arudishe haki hiyo kabla ya mauti kumfika binaadamu au sivyo itabidi ahesabiwe Akhera
Ikiwa hakuna uwezekano wa kumrudishia mtu haki yake, kama kuwa na khofu kuwa labda itamletea madhara zaidi, basi anatakiwa Muislamu aombe Maghfira na Tawbah, kisha baada ya kuacha kitendo hicho kabisa, azidishe mema yake na amfanyie wema yule mwenzake aliyemdhulumu na kumuombea maghfira na du'aa. Vile vile mnasihi na huyo fundi maana naye anashiriki kwenye wizi huo, na ni wangapi anaowasaidia kwenye wizi huo?? Mfikishie nasaha na mwambie amche Mwenyeezi Mungu.
Na Allah Anajua zaidi.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


