28-Wewe Pekee Tunakuabudu: Tawassul Za Shirki Kufru Na Bid’ah: Kutawassal Kwa Du'aa Ya Al-Fawz Wal-Qabuwl

 

إِيَّاكَ نَعْبُدُ وَإِيَّاكَ نَسْتَعِينُ

Wewe Pekee Tunakuabudu Na Wewe Pekee Tunakuomba Msaada

 

Tawassul Za Shirki Kufru Na Bid’ah

 

28-Kutawassal Kwa Du’aa Ya  "Al-Fawz Wal-Qabuwl"

 

 

 

 

 Al-Fawz Wal-Qubuwl -  الفوز والقبول

 

Du’aa hiyo iliyopewa jina la "Al-Fawz wal-Qabuwl" (Kufuzu na kutakabaliwa) ni du’aa ya uzushi iliyoandaliwa katika kijitabu kidogo kabisa ambayo imeenea katika jamii mbali mbali ikiwemo jamii yetu ya Kiswahili.  

 

Imaam Ash-Shawkaaniy amesema katika ‘Al-Fawaaid Al-Majmuw’ah’: “Hadiyth isemayo: “Hakuna mja wa kike wala wa kiume amwombe Allaah au atake kitu usiku wa ‘Arafah kwa du’aa hii nayo ni maneno kumi, ila Allaah Atampa, isipokuwa kukata ukoo au dhambi…ikikusudiwa duaa inayosema - Subhaana-LLadhiy fis-Samaai ‘Arshuhuu…“

 

Inadaiwa imesimuliwa na Al-‘Uqayliy kutoka kwa Ibn Mas’uwd. Usimulizi unaodaiwa ni marfuw’ lakini katika isnaad yake kuna ‘Uzrah bin Qays Al-Yahmadiy, ambaye ni dhaifu.

 

Imaam Al-Albaaniy (Rahimahu Allaah) amesema: “Du’aa hii yenye maneno (kumi) isomwe mara elfu usiku wa ‘Arafah; ni katika bid’ah za ‘Arafah. Ametaja hivyo katika Kitabu chake cha Manaasik Al-Hajj wal-‘Umrah na kitabu chake ‘Hajjatun-Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam)“ [Markaz Al-Fatwa namba 66019]

 

 

Du’aa hiyo ya uzushi ya Al-Fawza Wal-Qubuwl  inaanza kama ifuatavyo:

 

تعلموا هذا الدعاء فإنه تعلمه الأولياء والصالحون، فوالذي بعثني بالحق نبيا مادعا بهذا الدعاء أحد في عمره مرة واحده أو ساعه أو يوما أو شهرا إلا أدخله الله الجنه بلا حساب ولا عقاب وإن الملائكه يستغفرون له بأجمعهم ويصلون عليه، والذي بعثني بالحق بشيرا ونذيرا مادعا بهذا الدعاء مسلم في مفازه مخيفه إلا أمن ولا جائع إلا شبع ولا عريان إلاكساه الله ولا عطشان إلا رواه الله ولا مديون إلا قضى الله دينه ولا مكروب إلا فرج الله كربه ولا مغموم إلا أذهب الله غم.

 

"Jifunzeni du’aa hiyo kwani wamejifunza awliyaa na Swaalihiyna, kwani naapa kwa Ambaye Amenituma kuwa Nabiy, hakuna aombaye du’aa hii katika umri wake mara moja au saa moja, au siku moja au mwezi mmoja, isipokuwa Allaah Atamuingiza Jannah bila hesabu wala adhabu na Malaika wanamuombea maghfirah wote kwa umoja na wanamswalia. Naapa kwa Ambaye Amenituma kwa haki kuwa mbashiriaji na mwonyaji, hakuna Muislamu aliyekuwa katika khofu akaomba du’aa hii isipokuwa atakuwa katika amani, wala mwenye njaa isipokuwa atashiba, wala aliye uchi isipokuwa Allaah Atamvisha, wala mwenye kiu isipokuwa Allaah Atamnywesha, wala mwenye deni isipokuwa Allaah Atamkidhia deni lake, wala mwenye dhiki isipokuwa Allaah Atampa faraja kumtoa katika dhiki yake, wala mwenye ghamu (huzuni) isipokuwa Allaah Atamuondoshea ghamu yake…"

 

 

Du’aa hiyo ya uzushi ya Al-Fawz Wal-Qubuwl inaendelea mpaka inafikia kutaja:

 

 

من كتبه وجعله حرزا كفاه الله شر مايخافه ويحذره، ومن مات ثم جعله في عنقه كان له انيسا في قبره ووكل الله به ملائكه يحفظونه من كل سوء، ويكفيه الله شر منكر ونكير وما في يوم القيامه والملائكه عن يمينه وعن شماله ويجعله الله في أعلا عليين، ويبني له بيتا في الجنه من لؤلؤة بيضاء يرى باطنها من ظاهرها، ويفتح الله له مائة ألف باب في كل باب مائة ألف مدينه وفي كل مدينه مائة ألف قصر وفي كل قصر مائة ألف حجرة في كل حجرة مائة ألف زاويه في كل زاويه مائة ألف صفه في كل صفه مائة ألف سرير في كل سرير مائة ألف فراش في كل فراش مائة ألف حوريه لكل حوريه مائة ألف حلة معها كاس مملوء من شراب ، ثم ترفعه الملائكه على سرير من نور ويقبل الله عز وجل عليه من فوق العرش ثم يقول الله: ياعبدي أنا راض عليك بفضيلة هذا الدعاء.

"Atakayeiandika na kuifanya ni hirizi, Allaah Atamuondoshea shari anayokhofia na kuitahadhari, na atakayefariki kisha akaweka katika shingo yake, itakuwa ni kiliwazo katika kaburi lake, na Allaah Atamwakilishia Malaika wamhifadhi na kila ovu, na Allaah Atamtoshelezea shari za Munkar na Nakiyr (Malaika wawili watakaouliza wafu kaburini maswali matatu), na pia (Atamtosheleza) yale yaliyoko Siku ya Qiyaamah, na ambayo ya Malaika wa kuliani kwake na kushotoni kwake, na Allaah Atamjaalia awe miongoni mwa watu wa ‘Illiyyiyn (daraja ya juu kabisa ya watu wema), na Allaah Atamjengea nyumba huko Jannah ya lulu nyeupe ambayo inaonekana ndani yake kutoka nje yake, na Allaah Atamfungulia milango laki moja, kila mlango ataona miji laki moja na kila mji kuna maqasri (majumba ya fakhari) laki moja,  na kila qasri kuna vyumba laki moja na kila  chumba kuna kona laki moja, na kila kona kuna wanda (eneo, nafasi) laki moja na kila wanda kuna vitanda laki moja, na kila kitanda kina matandiko laki moja, na kila tandiko kuna mahuri (wanawake wazuri wa Jannah) laki moja, na kila huri ana mapambo ya thamani laki moja, na kila mmoja ana bilauri yenye kinywaji, kisha Malaika atamnyanyua kwenye kitanda kisha Allaah Atamkabili kutoka katika ‘Arshi Yake kisha Allaah Atasema: “Ee mja wangu, Mimi niko radhi nawe kwa fadhila ya du’aa hii..."

 

Du’aa yenyewe ya uzushi Al-Fawz Wal-Qubuwl  ni ifuatayo:

 

سبحان الذي في السماء عرشه، سبحان الذي في الأرض ملكه، سبحان الذي في الجنه رحمته، سبحان الذي في النار سلطانه، سبحان الذي في الهواء روحه، سبحان الذي في القبور قضاؤه، سبحان الذي لا منجا منه إلا إليه في الدنيا والآخره، سبحانك انت الله العزيز الحكيم، سبحانك انت الله رب العالمين، سبحانك انت الله الرحمن الرحيم، سبحانك انت الله الملك القدوس، سبحانك انت الله المؤمن المهيمن ، سبحانك انت الله الجبار المتكبر، سبحانك انت الله الخالق البارئ، سبحانك انت الله المصور الحكيم، سبحانك انت الله السميع العليم، سبحانك انت الله البصير الصادق، سبحانك انت الله اللطيف الواسع، سبحانك انت الله الولي الكبير، سبحانك انت الله البديع الاحد، سبحانك انت الله الغفور الودود، سبحانك انت الله الشكور الحميد، سبحانك انت الله الحميد المجيد، سبحانك انت الله المبدئ المعيد، سبحانك انت الله الأول الأخير، سبحانك انت الله الظاهر الباطن، سبحانك انت الله الوكيل الكافي، سبحانك انت الله الواحد الأحد، سبحانك انت الله الفرد الصمد، سبحانك انت الله القريب الدائم، سبحانك انت الله الحق المتعال، سبحانك انت الله الباعث الوارث، سبحانك انت الله الباقي الرزاق، سبحانك انت الله الحق المبين، سبحانك انت الله العزيز المجيب، سبحانك انت الله القابض الباسط، سبحانك انت الله الرزاق الفتاح، سبحانك انت الله الولي العلي، سبحانك انت الله البديع الصمد، سبحانك انت الله الحبيب البارئ، سبحانك انت الله ذو الجلال والإكرام، سبحانك انت الله الحي القيوم، سبحانك انت الله المحيي المميت، سبحانك انت الله الناظر الخالق، سبحانك انت الله العزيز الفتاح، سبحانك انت الله الحنان المنان ، سبحانك انت الله الشكور الديان، سبحانك انت الله القدير الغفار، سبحانك انت الله الصادق العدل، سبحانك انت الله الظاهر الباطن المتعال، سبحانك انت الله الرفيع الباقي سبحانك انت الله الوهاب المعطى، سبحانك انت الله الولي البصير، سبحانك انت الله الكفيل المستعان، سبحانك انت الله المنعم المتفضل، سبحانك انت الله أرحم الراحمين، سبحانك انت الله خير الفاصلين، سبحانك انت الله خير الناصرين، سبحانك انت الله خير القادرين، سبحانك انت الله خير الوارثين، سبحانك انت الله خير الزاهدين، سبحانك انت الله خير المعطين، سبحانك انت الله الرءوف الرحيم، سبحانك إني كنت من الظالمين .
فسيكفيكم الله وهو السميع العليم .

 

Basi tazama Muislamu jinsi uongo wa wazushi ulivyozidi hadi wanazusha katika mas-alah ya msingi ya ‘Aqiydah ya Muislamu; mas-alah ambayo yako wazi kuwa mwana Aadam hana uwezo wala madaraka nayo bali yako katika uwezo na mamlaka ya Allaah. Na mengineyo yaliyomo humo ndani wanayozusha ambayo ni katika mambo ya ghayb; hakuna mwenye ‘ilmu nayo isipokuwa Allaah pekee.

 

 

Tahadhari ee ndugu Muislmu ujiepushe na du’aa hiyo ya uzushi, kwa sababu:

 

1. Hapana shaka kwamba Hadiyth hiyo ni mawdhwuw’ (ya kutungwa) na makdhuwb (ya uongo).

 

 

2. Katika alama za uongo wake ni hayo malipo ya mwenye kusoma du’aa hiyo na kwamba Allaah Ataumba kadhaa wa kadhaa kwa ajili ya du’aa hii na idadi kubwa iliyotajwa ya hayo yatakayoumbwa na Allaah au Atakayoyatoa kama thawabu! Kama vile mahuril 'ayn laki moja!

 

 

3. Du’aa hiyo inaendelea kutajwa mengi ya uzushi kama kutajwa kwamba msomaji du’aa hiyo atapata thawabu za Malaika wanne na thawabu za Manabii wanne! Na pia inadaiwa kuwa atakayeibiwa kitu basi atakipata kitu alichoibiwa. Na baya zaidi ni kutaja ya kumshirikisha Allaah kuhusu kuandikwa kwake katika hirizi, jambo ambalo ni ubatilifu na shirki katika Uislamu na linafikia kumtoa mtu nje ya Uislamu! 

 

 

4. Kueneza Hadiyth za kumzulia Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ni khatari kwa Muislamu kuwa makazi yake yatakuwa ni motoni na kwamba ni dhambi kubwa, na kwamba atakayeeneza atabeba dhambi za kila atakayeisoma du’aa hiyo kwa dalili kwamba Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

((مَنْ كَذَبَ عَلَيَّ مُتَعَمِّدًا فَلْيَتَبَوَّأْ مَقْعَدَهُ مِنْ النَّارِ)) البخاري

((Atakayenizulia uongo kwa makusudi, basi ajiandalie makazi yake motoni [Al-Bukhaariy]

 

 

5. Hakuna shaka kwamba anayemuongopea Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) atakuwa ni mwenye kuwaongopea wenzake; amesema Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam):

 

مَنْ حَدَّثَ عَنِّي حَدِيثًا وَهُوَ يَرَى أَنَّهُ كَذِبٌ، فَهُوَ أَحَدُ الْكَاذِبَيْنِ

(Atakayezua Hadiyth kutoka kwangu akijua kuwa  ni ya uongo basi yeye ni mmoja wa waongo wawili)) (Aliyeizua na anayeendelea kuizua) [Muslim katika Muqaddimah ya Swahiyh yake]

 

Basi haijuzu kuieneza Hadiyth hiyo, wala kuitaja fadhila zake, wala kuifanyia kazi wala haipasi kuitaja kabisa kuwa ni Hadiyth bali tunasema ni maneno ya uzushi kutoka kwa wazushi! 

 

 

 

Share