Riba Inayotokana Na Kuwekeza Katika Saccos
SWALI:
Assalaam Allaykum
Ninapenda kuuliza ya kuwa kwa sasa kumezuka mpango kuanzisha saccos yaani watu watu wanaunda kikundi chao na wanaweka pesa na baadaye mwanachama anakopa na anaporejesha anatakiwa arejeshe na riba.Ile riba inakuwa ndiyo gharama ya kuendeshea chama/kikundi na mwisho mwaka wanaangalia kiasi cha matumizi na kiasi cha riba kilichobakia wanagawana kutokana na hisa ya mwanachama Sasa kwa kuwa kila mwanachama anafaidika na hiyo riba je itakuwa ni halali kujiunga na vikundi kama hivi? Naomba majibu ili nielimike kwa
Mwanyezi Mungu tunakuomba utunusuru na ghadhabu yako, utujaliye yaliyo mema
Ni ndugu yenu katika Uislamu
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukran ndugu yetu katika Iymaan kwa suala lako
Hakika ni kuwa Allaah Aliyetukuka Ametangaza vita na yeyote anaye chukua riba pale Aliposema: “Enyi mlioamini! Mcheni Allaah, na acheni riba zilizobakia, ikiwa nyinyi ni Waumini. Basi mkitofanya jitangazieni vita na Allaah na Mtume wake. Na mkitubu, basi haki yenu ni rasilmali zenu. Msidhulumu wala msidhulumiwe” (2: 278 – 279).
Baadhi ya wajinga wanakuwa ni wenye kulinganisha baina ya riba na faida ya biashara kwa hivyo zote mbili hazina matatizo na ni halali. Allaah Aliyetukuka Anawajibu: “Biashara ni
Ni hakika kuwa pesa za sadaka huvia na za riba hunywea na kuleta hasara kwa mwenye kukengeuka na amri ya Allaah. Allaah Aliyetukuka Anasema: “Allaah huiondolea baraka riba, na huzibariki sadaka. Na Allaah hampendi kila mwenye kukanya na afanyae dhambi” (2: 276).
Kuchukua mikopo ya riba ikiwa ni kutoka kwa mtu binafsi, shirika, saccos, banki na kadhalika zote ni haramu. Kila mmoja atazame hasara inayopatikana hapa duniani kwa watu hao ambao wanakiuka amri za Allaah na kesho Akhera watakuwa na adhabu kali zaidi. Na Mtume (Swalla Llaahu 'alayhi wa sallam) ametuambia: “Dirhamu (pesa za fedha) moja ya riba ambayo mtu anaila kwa kujua ni mbaya zaidi kuliko kuzini mara thelathini na sita [36]” (Ahmad).
Ni nasiha zetu kwa ndugu zetu katika Iymaan wakiepushe kabisa na muamala wowote ambao ni wa riba. Tukifanya hivyo bila shaka Allaah Aliyetukuka Atatutolea njia katika mambo yetu. Allaah Aliyetukuka Anasema: “Na anayemcha Allaah Humtengezea njia ya kutokea. Na humruzuku kwa njiya asiyotazamia. Na anayemtegemea Allaah Yeye humtosha” (65: 2 – 3).
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha
