128-Aayah Na Mafunzo: Tukio La Kuumizwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Katika Vita Vya Uhud

 

Aayah Na Mafunzo

Aal-‘Imraan

Tukio La Kuumizwa Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) Katika Vita Vya Uhud

Alhidaaya.com

Anasema Allaah (سبحانه وتعالى):

لَيْسَ لَكَ مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ أَوْ يَتُوبَ عَلَيْهِمْ أَوْ يُعَذِّبَهُمْ فَإِنَّهُمْ ظَالِمُونَ ﴿١٢٨﴾

Si juu yako katika jambo hili; ima Apokee tawbah yao au Awaadhibu, kwani wao ni madhalimu. [Aal-'Imraan: 128]

 

 

Mafunzo:

 

Sababun-Nuzuwl: 

 

Aayah hii imeteremka kama alivyohadithia Ibn ‘Umar (رضي الله عنه) kwamba: Alimsikia Nabiy (صلى الله عليه وآله وسلم) alipoinua kichwa chake kutoka rukuu’ ya mwisho ya Swalaah ya Alfajiri baada ya kusema:

سَمِعَ اَللَّهُ لِمَنْ حَمِدَه رَبَّنَا لَكَ اَلْحَمْدُ

“Sami’a-Allaahu liman hamidah Rabbanaa Lakal-Hamd.  

Allaah Amemsikia aliyemhimidi, Ee Rabb wetu, Himdi ni Zako Wewe

 

 

 Kisha akasema:

اللَّهُمَّ الْعَنْ فُلَانًا وفُلَانًا وفُلَانًا

“Allaahumma mlaani fulani na fulani na fulani.” Ikateremka:

 

لَيْسَ لَكَ مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ أَوْ يَتُوبَ عَلَيْهِمْ أَوْ يُعَذِّبَهُمْ فَإِنَّهُمْ ظَالِمُونَ ﴿١٢٨﴾

 

Jambo hili halikuhusu wewe; ima Apokee tawbah yao au Awaadhibu, kwani wao ni madhalimu. (3:128). [Al-Bukhaariy na wengineo kwa riwayaah nyenginezo]

 

 

Na Anas bin Maalik  (رضي الله عنه) amehadithia kwamba: Siku ya Uhud, jino la Rasuli wa Allaah (صلى الله عليه وآله وسلم) lilivunjika na akachomwa mkuki begani mwake. Damu ikawa inamchirizika usoni mwake akawa anaifuta damu huku akisema: “Vipi watu watafaulu ikiwa wamerowanisha uso wa Nabiy wao kwa damu na hali yeye anawalingaia kwa Allaah?” Hapo ikateremka Aayah hii:

 

لَيْسَ لَكَ مِنَ الْأَمْرِ شَيْءٌ أَوْ يَتُوبَ عَلَيْهِمْ أَوْ يُعَذِّبَهُمْ فَإِنَّهُمْ ظَالِمُونَ ﴿١٢٨﴾

 

Jambo hili halikuhusu wewe; ima Apokee tawbah yao au Awaadhibu, kwani wao ni madhalimu” (3: 128) [At-Tirmidhiy Hadiyth Hasan Swahiyh].

 

Share