02-Imaam Ibn ‘Uthyamiyn: Kufuturu Tende Kwa Idadi Ya Witr

Kufuturu Tende Kwa Idadi Ya Witr

 

Imaam Ibn ‘Uthyamiyn (Rahimahu-Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

SWALI:

 

Nimesikia kwammba mwenye swawm anawajibika pale anapofuturu tende, iwe ni idadi ya witr yaani iwe tano au saba  na kadhaalika Je ni waajib?

 

JIBU:

 

Si waajib, bali hata sio Sunnah mtu afuturu kwa witr; tatu au tano au saba au tisa isipokuwa Siku ya ‘Iyd kwani imethibiti kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alikuwa hatoki kwenda Swalaah Siku ya ‘Iydul-Fitwr mpaka ale kwanza tamar (tende) na alikuwa akila kwa witr. 

Ama nje ya hayo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) hakukusudia kula tende kwa witr.

 [Fataawa Nuwr ‘Alad-Darb 11/2]

 

 

 

Share