006-Swahiyh Twibbin-Nabawiy: Tiba Ya Kiwiliwili Imegawanyika Katika Sehemu Mbili

 

 

Swahiyh Twibbin Nabawiy

 

006- Tiba Ya Kiwiliwili Imegawanyika Katika Sehemu Mbili

 

 

 

 

Ya kwanza:

 

Aina ambayo Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Amewaumbia wanyama wanaonena na wanyama wasionena; aina hii haihitajii matibabu ya tabibu; kama tiba ya njaa, kiu, baridi, uchovu, kwa kuelekea dhidi ya shida hizo na kuziondoa.

 

 

Aina ya pili inayohitajia kufikiria na kuzingatia kwa makini. Kama kutibu maradhi yanayoshabihiana yanayotokana na hali ya hisia ya nafsi inayomtoa mtu katika hali yake ya sawasawa, na kuelekea ima kwenye harara au baridi au yabisi, au unyevunyevu, au yanayokutana mawili katika hali hizo nazo ni aina mbili: Ima ni ya kimaada au ni hali isiyo maada. Yaani: Ima kuwa katika kumiminika maada, au kwa kuzuka, hali ya tofauti kati ya maradhi hayo ni maradhi ya kihali (kayfiyyah) hutokea baada ya kuondoka maada zilizozisababisha, hapo huondoka na maada yake na athari yake kubakia katika hisia.

 

 

Maradhi ya ki-maada zina sababu zake, na ikiwa sababu za maradhi pamoja nayo; basi atakayeangalia sababu hiyo inapasa kuanguka kwanza kisha pili huangalia maradhi, kisha la tatu kuangalia dawa.

 

 

Ama maradhi ya vifundo ni yale maradhi ambayo yanamuondosha mtu kiungo chake na kubadilsha umbo, ima katika umbo, au kwa kuminya, au kwa kupita, au kwa kuguswa au mfupa au kiunguo. Viungo vyote hivi, ikiwa vitaungana na kuitwa viwiliwili vitashikamana: Ama kuungana na kuachana kutoka katika hali ya kawaida huitwa: Kuachana, kukatika au maradhi ya jumla ambazo yanazikutanisha zilizoshabihiana na hizi za viungo.

 

Ama maradhi yanayoshabihiana, ni yale maradhi ambayo huondosha uchangamfu wa mtu wa kawaida (hali yake ya sawasawa). Nayo ni ambayo huondosha hali ya kawaida ya kiungo, ima katika umbo, au kuingiza uwazi, au mwendo, au ugumu, au kuwa laini, au idadi, au ukubwa, au muonekano, viungo hivi ikishikamana na kuunda kiwiliwii, huitwa muungano huo muungano wa mwili. Ama kutoka kwenye hali ya sawa sawa huitwa kukawanyika kwa muungano wa kimwili. Au maradhi ya jumla yanayo jumuisha yanayoshabihiana na ya viungo.

 

 

Maradhi yanayoshabihiana, ni yanayoitoa nafsi katika hisia ya sawasawa, kuitwa ugonjwa ni pale yatokapodhuru kwa dhahiri. Maradhi haya yako katika aina nane: Manne ni mepesi na manne ni muunganiko wa zaidi ya moja.

 

 

Mepesi (moja moja) ni: baridi, joto, rutuba, yabisi.

 

Muunganiko: Joto na rutuba, joto na yabisi, baridi na rutuba na baridi na yabisi.

 

Maradhi haya ima huwa kwa sababu ya kumiminika maada, au bila kumiminika maada, na kama hakuna madhara ya dhahiri huitwa, ni kutoweka katika hali ya afya iliyo sawa.

 

Mwili una hali tatu:

 

a-Hali ya kimaumbile

b-Hali iliyo nje ya kimaumbile

c-Hali ya kati na kati.

 

 

Ya Kwanza: Mwili huwa na afya.

 

Ya Pili: Mwili huugua.

 

Ya Tatu: Mwili huwa kati ya hali mbili hizo.

 

 

Hali hiyo ya tatu ni ya kati na kati; dhidi ya mbili hazigusi moja kwenda kwa mwengine, na mwili kutoka katika hali ya maumbile yake ya kawaida sababu yake ni ima ni kutokea ndani yake, kwani mwili ni muunganiko wa joto, baridi, rutuba, na yabisi, na ima kutokea nje kwani hukutana na kitu kinachoafikiana au kisichoafikiana, na madhara yanayomkuta mwana Aadam hutokana na hisia mbaya kutoka katika mstari wa sawa kiafya.

 

 

Au kutoka na uharibifu wa kiungo au kutokana na udhaifu wa nguvu, au roho zinazoibeba. Na hutokana na kuzidi, au kupungua au kufarikiana, au kuungana au kuendelea wakati mwili uko tofauti na hali hizo na kutoweka ulinganifu. Au kuwa nje ya umbo na kufanya kutoka katika ulinganifu wake ulio sawa.

 

 

Basi tabibu: Ni mtu anayetofautisha vitu ambavyo vikikutana humdhuru mwana Aadam.

 

 

Tabibu ni yule anayetenganisha vinavyomdhuru mwana Aadam ikiwa vitaunganishwa. Au anakusanya kwa mwana Aadam ile ambayo endapo vitatengana vitamdhuru mwana Aadam. Au humuongezea mtu ambayo humdhuru ikiwa vitapungua hapo huleta afya iliyokosekana, au kulinda kwa namna ilivyo au mfano wake na kuondosha shida iliyopo kwa kuleta hali tofauti, huiondosha shida hiyo kwa kizuizi cha kutoka hali hiyo kupitia  الحمية (himaya, kinga). Haya yote utayaona katika mwongozo wa Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kwa namna ya kukidhi haja na kutosheleza kabisa yatatimia haya kwa hila, nguvu fadhila na msaada kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa).

 

 

Share