008-Swahiyh Twibbin-Nabawiy: Kila Maradhi Yana Dawa Yake

 

 

Swahiyh Twibbin-Nabawiy

 

008-Kila Maradhi Yana Dawa Yake

 

 

 

Amepokea Imaam Muslim katika sahihi yake. Hadiyth ya Jaabir bin Abdillaah kutoka kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) kuwa amesema:

 

 

   ‏ ((لِكُلِّ دَاءٍ دَوَاءٌ فَإِذَا أُصِيبَ دَوَاءُ الدَّاءِ بَرَأَ بِإِذْنِ اللَّهِ عَزَّ وَجَلَّ)) ‏ ‏

 “Kila ugonjwa una dawa, ikipatiwa  dawa ya ugonjwa, hupona kwa idhini ya Allaah ‘Azza wa Jalla.”

 

Na Al-Bukhaariy (5678) kutoka kwa Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) amesema: Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

 

((مَا أَنْزَلَ اللَّهُ دَاءً إِلاَّ أَنْزَلَ لَهُ شِفَاءً)) ‏

“Allaah Hajateremsha ugonjwa wowote ila, ameteremsha na tiba yake.”

 

 

Na katika “Musnad Al-Imaam Ahmad” kutoka Hadiyth ya Usaamah bin Shariyk amesema:

 

كنتُ عندَ النبىِّ صلى الله عليه وسلم، وجاءت الأعرابُ، فقالوا: يا رسول الله؛ أَنَتَدَاوَى؟ فقال :((نَعَمْ يا عبادَ اللهِ تَدَاوَوْا، فإنَّ اللهَ عَزَّ وجَلَّ لم يضَعْ داءً إلا وَضَعَ لَهُ شِفاءً غيرَ داءٍ واحدٍ)) قالوا: ما هو ؟ قال: ((الهَرَمُ))

Nilikuwa kwa Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wakaja mabedui wakasema: Ee Rasuli wa Allaah, je, hujitibu? Akasema: “Naam, enyi waja wa Allaah jitibuni, kwani Allah ‘Azza wa Jalla Hajaweka ugonjwa ila pia Ameweka na tiba yake, isipokuwa ugonjwa mmoja tu”. Wakasema ni ugonjwa gani huo? Akasema: “Ukongwe”

 

na katika lafudhi nyingine,

 

 ((إنَّ اللهَ لم يُنْزِلْ دَاءً إلا أنزل له شِفَاءً، عَلِمَهُ مَنْ عَلِمَهُ، وَجَهِلَهُ مَنْ جَهِلَهُ))

“Hakika Allaah Hateremshi ugonjwa, ila Ameuteremshia tiba yake wameijua walioijua, na hawakuijua wasiyoijua.”

 

 

Hadiyth hizi ndani yake kuna kuthibitishia sababu na visababishi, na kubatilisha kauli ya anayekanusha. Yajuzu kuwa aliposema: “Kila ugonjwa una dawa.“ ni kwa ujumla wake inajumuisha pia hata magonjwa yanayoua na magonjwa ambao tabibu hawezi kuyatibu na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Amejalia tiba ya kuyaponyesha, lakini Amefunika elimu yake kwa watu kuweza kuifikia. Kwani viumbe hawana ujuzi wowote isipokuwa ule waliofundishwa na Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa). Kwa ajili hii, Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ameweka sharti la kupona katika kusadifu kukubaliana kwa dawa na ugonjwa. Kwani hakuna chochote katika viumbe isipokuwa dhidi yake kipo vile vile. Hivyo kila ugonjwa una dhidi yake ya dawa inayoutibu huo ugonjwa. Hivyo Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akaambatanisha kupona kwa maradhi na kuafikiana kwa ugonjwa na dawa. Na hiki ni kiasi kilicho sawa na ugonjwa, dawa inapovuka kiwango cha ugonjwa katika namna ya kutibia, au kiasi cha kutibia, ikawa zaidi ya inavyotakiwa, dawa italeta ugonjwa mwingine. Pia dawa ikiwa pungufu, haitaweza kupambana na maradhi pia matibabu yatakuwa na kasoro. Na hapo matibabu hayatakuwapo kama dawa hailingani na mgonjwa, au dawa haijakutana na ugonjwa tiba haitapatikana, na pindi muda ukiwa sio muwafaka kwa dawa hiyo basi haitofaa, mwili kama haukubaliani na dawa, au hakuna nguvu ya kuhimili dawa. Au kuna kizuizi chochote, basi kupona hakutakuwepo, ikiwa hayajasadifu mambo hayo, na yakipatikana hayo kusadifu kukutana basi na ponya kwa idhini ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) itatokea na hapana budi. Na maana hii ya Hadiyth ndio bora kati ya maana mbili.

 

Pili, Hadiyth ni katika kauli za jumla yenye muradi wa maana mahsusi hasa na hasa yanaoingia katika kauli, ni maradufu, maradufu ya maana iliyo nje.

Hii inatumika katika kila lugha na muradi unakuwa: kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Hajaweka ugonjwa unaotibika, ila Ameuwekea dawa. Hapa maradhi yale yasiyotibika hayaingii katika maana hiyo. Na hii kama kauli yake Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kuhusu upepo alioupeleka kwa kaumu ‘Aad.

 

تُدَمِّرُ كُلَّ شَيْءٍ بِأَمْرِ رَبِّهَا  

  Unadamirisha kila kitu kwa amri ya Rabb wake.  [al-Ahqaab: 25]

 

yaani, kila kitu kinachokubali kuteketea, ambacho kawaida upepo huweza kukiangamiza, na mifano ya hivyo ni mingi.

 

 

Na mwenye kuzingatia maumbile ya vitu vilivyo dhidi hapa Ulimwenguni, na kupingana, na vingine kuzuiana. Vingine kuishinda, mtu huyo atakumbuka hekima ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) na ufundi Wake katika Ar-Rubuwbiyyah (Uola Wake) na Upekee Wake (Subhaanahu wa Ta’aalaa) katika sifa Zake za ulezi, kuteza nguvu kila kitu. Yeye Ndiye Mmoja Pekee, lakini vingine vyote kila kimoja kina dhidi, na kwamba Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) ni Mkwasi kwa dhati Yake, na kila asiyekuwa Allaah anamuhitajia Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa).

 

 

Na katika Hadiyth zilizo sahihi ipo amri ya tiba. Na kwamba hilo halipingani na kutawakali kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa).

 

 

Kama ilivyokuwa kupambana na shida ya njaa, kifo, joto, baridi, na kuleta dhidi ya hiyo, yaani shibe kukata kiu, kuleta baridi, au joto, si kupingana na kutawakali kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa). Bali haitimii hakika ya Tawhiyd isipokuwa kwa kushikamana na sababu Alizoweka Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) kwa makadirio na ki-Shariy’ah, na kuziacha. huharibu tawakkul, pia inatofautiana na amri na hekima, na kuzidhoofisha, wakati asiyeshikamana na sababu anadhani, kuwa kule kuziacha kunatia nguvu zaidi katika kutawakali kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa).    Basi kumbe kuziacha kwa ajizi kunapingana na “Tawakkul” (Kumtegemea Allaah Subhaanahu wa Ta’aalaa) ambayo hakika yake moyo wa kutawakali kwa Allaah ni mjs kupata manufaa katika Dini yake na dunia yake na kuondosha madhara kwenye Dini yake na dunia yake, na katika kufanya hivyo hapana budi kushikamana na sababu kama sivyo itakuwa ameachilia kutofanya kazi, kwa hekima na shariy’ah, basi mja asifanye ile ajizi yake ndio, “Tawakkul” wala “Tawakkul” isiwe ni ajizi.

 

 

Katika haya, kuna radd kwa wale wanaokanusha kufaa kujitibia wakasema: “Kama kupona ni jambo limo katika Qadari ya Allaah basi kujitibu hakufai kitu, pia ikiwa haijakadiriwa kupona, vile vile hakuna maana ya kujitibia.”  Pia wanasema: “Maradhi yamepatikana kwa Qadari ya Allaah na Qadari ya Allaah haipangwi wala hairudishwi nyuma.”

 

 

Na swali hili ndilo ambalo wale mabedui walimuuliza Rasuli wa Allaah (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Ama Maswahaba watukkufu (Radhwiya Allaahu ‘anhum) watukufu, ni wajuzi zaidi wa Allaah na hekima Zake na sifa Zake wasingeweza kuuuliza swali kama hilo. Na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alishawajibu wale mabedui majibu kamili, yanayotosheleza. Akasema:  Madawa haya na ruqya na taqwa ni miongoni mwa Qadar za Allaah, basi haindoki kitu katika Qadar Yake, bali Qadar yake inarudisha Qadar nyingine. Na jibu hili ni katika Qadar Yake, na hili ni kama jibu la mwenye njaa, kiu, joto na baridi na kinyume chake, ni kama jibu la Qadar ya adui katika jihaad, na kila ambaye Allaah Anamuandikia ni Yule anayesukuma, anayesukumwa na kisukumo chenyewe.

 

 

Husemwa kwa mwenye kuuliza swali hili: Hii yakupasa kutofanya sababu yoyote katika sababu yenye kukuletea manufaaa na kukuondoshea madhara; kwa kuwa manufaaa na madhara ni makadirio yetu tuliyokadiriwa; hayakuwa na budi isipokuwa kutokea kwake, na hata kama hayajakadiriwa; basi yasingetokea, na hili ni kuharibu Dini na dunia kwa pamoja na kuharibu ulimwengu. Halisemi hili ila yule mpinga haki na mwenye inadi. Hutaja Qadar ili tu apinge hoja; kama vile washirikina walivyosema:

 

  لَوْ شَاءَ اللَّـهُ مَا أَشْرَكْنَا وَلَا آبَاؤُنَا

 “Lau Allaah Angetaka, tusingelifanya shirki, wala baba zetu” [Al-An’aam: 148]

 

 

Hili wamelisema kama kutetea hoja zao kwa Allaah juu ya Mitume.

 

 

Jibu la swali hili: Ni kusemwa: imebakia sehemu ya tatu ambayo hakutaja, nayo ni kuwa: “Allaah Amekadiria kadha wa kadha kwa sababu hii, ikija sababu basi itatokea kilichosababishwa, vinginevyo.” Hapana! Kwa mfano akisema: “Ikiwa nitakuwa nimekadiriwa sababu; nimefanya na kama haikukadiria kwangu; sitoweza kusema.” Je hoja hii itakubaliwa kwa mtumishi wako, na mtoto wako, na kukulipa ikiwa atatoa hoja kwako kwa kile ulichokiteremsha na kukikataza; na kuwa kinyume chako?

 

 

Utakapokutana nae; itakubaliwa vipi kwako katika kutetea haki za Allaah juu yako. Na katika kauli yake Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) aliposema: “Kila ugonjwa una dawa.” Ni kumpa nguvu mgonjwa na tabibu, na akahimiza ili watu watafute hiyo dawa. Wafanye utafiti na kugundua dawa.

 

 

Mgonjwa anapohisi kuwa ule ugonjwa wake unayo dawa utakaouondosha; basi moyo wake utapata matumaini na kasi ya kukata tamaa itapoa, mlango wa matumaini utamfunukia nafsi yake inapopata nguvu, joto lake la kimaumbile huibuka na kwa hiyo huwa sababu ya kuibuka joto lake la kimaumbile na hiyo huwa ni sababu ya nguvu ya roho za kihayawani, kinafsi, na kitabia ya kimaumbile, na roho hizi zinapopata nguvu, basi huimarika nguvu zinazoibeba na kuyashinda maradhi na kuyaondoa kabisa.

 

 

Kadhalika tabibu anapojua kuwa ugonjwa huu unayo dawa hapo, ataweza kuitafuta na kuifanyia uchunguzi.

 

 

Maradhi ya viwiliwili yako katika vipimo vya maradhi ya nyoyo, Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Hajafanya maradhi ya nyoyo ila pia Ameyafanyia “Shifaa” (ponya lake) kwa namna iliyo dhidi yake. Mgonjwa akijua hilo akatumia, na ikasadifu ugonjwa wa moyo wake itamponyesha kwa idhini ya Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa).

 

 

 

Share