010-Swahiyh Twibbin-Nabawiy: Maradhi Ya Kiwiliwili Kujikinga Na Kuvimbiwa Na Kula Kulingana Na Haja

Swahiyh Twibbin-Nabawiy

 

010-Maradhi Ya Kiwiliwili Kujikinga Na Kuvimbiwa

Na Kula Kulingana Na Haja.

 

 

 

Maradhi ni aina mbili: Maradhi ya kimaada, hutokana na kuongezeka kwa maada, imepitiliza kiwango kwenye mwili hadi ikadhuru utendaji wake wa kawaida na maradhi ya namna hii ni mengi yaliyokithiri na sababu yake: Kuingiza chakula mwilini kabla ya kuyeyushwa cha kwanza tumboni. Na kuzidisha kiasi kinachotakiwa na mwili. Pia kula vyakula vyenye virutubisho vichache. Vinavyosagwa polepole, na kula vyakula vingi kwa pamoja vyenye aina na mifumo mbali mbali. Binaadamu akijaza tumbo lake vyakula vya namna hii, akazowea kufanya hivyo, hiyo itamletea maradhi anuwai, kati ya hayo kupona kwake ni polepole, na mengine hupona haraka. Binaadamu akila ulaji wa wastani, akatumia kiwango kinachohitajia mwili kwa namna ya kiwango cha wastani na aina nzuri mwili huwa unafaidika zaidi kuliko kula sana.

 

Chakula kina ngazi tatu:

 Ya kwanza ni haja.

Ya pili ni kutosha.

Ya tatu yake ni ziada.

 

Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ameeleza kuwa mtu vinamtosha vitonge vya kusaidia kunyoosha mgongo wake ili asiishiwe na nguvu, asidhoofike, akivuka kiasi hicho basi ale kiasi cha kujaza theluthi ya tumbo lake. Na theluthi nyingine aziache kwa maji na ya tatu, iwe kwa ajili ya kupumua vizuri. Na mwongozo huu una faida sana kwa mwili na moyo. Kwani tumbo linapojaa chakula huwa finyu katika kunywa maji na ikipata kinywaji basi hufinyika katika nafsi ya kupumua. Hapo huwa ni shida sana kama vile mtu aliyebeba mzigo mzito. Jambo hilo hufisidi moyo na viungo vyote kushindwa kuleta utiifu wa ‘ibaadah mbalimbali, na badala yake hujishughulisha na utashi wa matamanio unaotokana na kushiba mno.

 

Hivyo kujaza tumbo kwa chakula hudhuru moyo na mwili[1].  Hili likiwa linafanyika mara kwa mara (yaani mara nyingi), ama ikiwa mara moja moja basi haina madhara, kwani mara moja Swahaba Abuu Hurayrah (Radhwiya Allaahu 'anhu) alikunywa maziwa mbele ya Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ((Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), kiasi cha kusema: “Kwa hakika Yule aliyekutuma kwa haki simpatii njia.”[2]  Na mara nyingi Maswahaba walikula na kushiba na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) yupo nao pamoja.

 

Kushiba kupindukia hudhoofisha nguvu na mwili, japo hurutubisha, kwani mwili hupata nguvu kulingana na anavyokula, na sio wingi wa chakula.

 

Kwa kuwa Mwanadamu sehemu yake moja ni ya ardhi, nyengine ya hewa, na nyingine ya maji. Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amegawa chakula cha Mwana Aadam na kinywaji chake na nafsi yake mafungu matatu.

 

Pakisemwa iko wapi fungu la sehemu ya

kimoto?

 Jibu: Haya ni mambo ambayo wameyaongelea matabibu. Na kusema, “Kwenye mwili kuna sehemu ya kimoto hasa na ni mojawapo ya nguzo na asili yake”.  Wamepingwa na matabibu wengine. Na wengine wasio matabibu, kwa kusema kuwa: “Mwilini hakika hakuna sehemu ya kimoto” na wametegemea hoja mbali mbali kama ifuatavyo:

 

Ya Kwanza: Kwamba hiyo sehemu ya kimoto ima yaweza kusemwa kuwa imedondoka kutokana na “athiyr” na kuchanganyika na sehemu za kimaji na kiardhi, au itasemwa kwamba imefanya humo na ya kwanza katika namna mbili haikubaliki.  

 

Mojawapo ni kuwa moto daima kwa tabia yake ni wenye kupanda na kushuka basi ni kutokana na nguvu ya kulazimisha kutoka kwenye kutoka kwenye kituo chake na kuja Ulimwenguni.

 

Ya Pili kwamba ingebidi moto upite kwenye mzingo baridi mno kushuka chini, nasi tunaona kuwa hapa Ulimwenguni moto huzimika kwa maji kiasi kidogo tu, basi kiasi cha moto mdogo kupita katika mkusanyiko wa baridi kali mno, ni aula zaidi kuzimika.

 

Na ya Tatu, ni kusemwa kuwa:  Kuwa moto umefanyika hapa hapa, hilo ndio halikubaliki zaidi. Kwani mwili uliogeuka moto baada ya kutokuwa hivyo, hapo kabla ulikuwa ima, ardhi, na ima maji, au hewa. Kwani nguzo za asili ya vitu ni hizo nne tu. Na hiki kilichogeuka kuwa moto, kwanza, kilikuwa kimechanganyika na mojawapo ya vitu hivi, na kuungana pamoja kabisa. Na kitu ambalo sio moto, kikikutana na vitu vyenye maumbo makubwa visivyokuwa moto, hakiwezi kuwa katika uelekeo wa kuwa moto. Kwani chenyewe sio moto. Na maumbo ya vitu baridi mchanganyiko, vipi vitakuwa katika utayari wa kugeuka kuwa moto?

 

Mkisema: Kwa nini kusiwepo sehemu za tabia ya moto kuweza kugeuza maumbo ya kuyafanya kuwa ni moto, kwa kule kufanyika nayo.

 

Tunasema kuwa kuzungumzia kuwepo kwa hizo sehemu zenye tabia ya kimoto, kama kuzungumzia maelezo yaliyopita hapo awali. Kama mtasema: Tunaona kurashiza maji kwenye chokaa inayozima moto hujitenga na hiyo chokaa mwanga wa jua ukichoma kwenye maada ya kioo, moto hujitokea, tukipiga jiwe juu ya chuma moto hujitokeza, na tabia zote hizi za kimoto hutokea wakati wa kuchanganyika. Na hii linabatilisha mliyoyasema kwenye sehemu ya kwanza vile vile.

 

Wanaokanusha wanasema: Sisi hatukanushi kuwa kiponda kikubwa huzusha moto, kama vile kuponda mawe juu ya chuma, au nguvu ya kupasha moto kupitia jua huleta moto kama katika kioo, lakini tunasema haiwezekani kabisa hilo kutokea katika vitu vyenye maumbo ya mimea na wanyama hata kuleta moto. Pia hakuna ule usafi, na mng’aro unaofikia kiwango cha kioo. Vipi miali ya jua inamulika juu yake, na moto hautokei kabisa. Basi mwanga unaofika ndani yake utawezaje kuzua moto?

 

Namna ya pili: Katika hoja ya msingi: Matabibu wamekubaliana kwa pamoja maji ya kale yenye joto kali mno, kama vijisehemu vya tabia ya joto ndiyo sababu ya hilo joto linalopakaa kwenye maji ingekuwa ni muhali. Sababu sehemu za moto japo kidogo inaingiaje akilini kuwa itabakia ndani ya sehemu za maji mengi kitambo cha bahari, bila kuzimika, karne kwa karne wakati tunaona kitabia moto mkubwa huzimwa kwa maji machache.

 

Namna ya Tatu: Kama mnyama na mmea ni sehemu ya moto imo ndani yao hasa, ingezidiwa na sehemu ile ya maji iliyomo ndani yao, na kushinda chembe hufanya zile tabia za chembe iliyoshinda igeuze chembe iliyoshindwa, hivyo lazima vichembe vya moto vichache vingegeuka na kufuata tabia ya maji ambayo ni dhidi ya moto.

 

Namna ya Nne: Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametaja kuumbwa kwa mwana Aadam katika mahali pengi ndani ya Qur-aan.

 

Anamuelezea mwana Aadam kuwa ameumbwa kutokana na maji, na sehemu nyingine Anamulezea kutokana na udongo, na katika baadhi ya Aayah nyengine kuwa ameumbwa kwa mchanganyiko wa viwili hivyo ambao ni tope. Sehemu nyingine Anamuelezea kuwa Amemuumba kutokana na udongo mfinyanzi uliokauka, utoao sauti kama kigae; udongo huu umepigwa jua na upepo mpaka ukageuka kigae, na hakuna mahali popote ambapo Anapoelezea kuwa mwana Aadam aliumbwa kwa moto, bali amejaalia hiyo kuwa ni sifa mahsusi kwa iblisi.

 

Na imethibiti katika Swahiyh Muslim kwamba Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:

خُلِقَتِ الْمَلاَئِكَةُ مِنْ نُورٍ وَخُلِقَ الْجَانُّ مِنْ مَارِجٍ مِنْ نَارٍ وَخُلِقَ آدَمُ مِمَّا وُصِفَ لَكُمْ  

“Malaika wameumbwa kwa nuru, na majini wameumbwa kwa miali ya moto, na Aadam ameumbwa kutokana na mlivyoelezwa.” [Swahiyh Muslim (2996) kutokana na Hadiyth ya ‘Aaishah Radhwiya Allaahu ‘anhaa]

 

Na hili ni wazi kwamba Aadam  ameumbwa kwa kile kilivyoelezwa ndani ya Qur-aan tu na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa)    Hajatuelezea kwamba Amemuumba kutokana na moto wala katika maada zake kuna chembe ya moto.

 

Namna ya Tano: Upeo wa dalili yao ni joto la miili ya wanyama, kwamba ni dalili ya kuwepo visehemu vya moto. Wakati hiyo sio dalili. Kwani sababu za joto ziko zaidi ya moto, wakati mwengine hutokana na moto, na mara nyingine hutokana na harakati na kutokana na kuakisi miali, na ujoto wa hewa, na kuwa jirani na moto, na hii ni kutokana na joto kali la hewa – vile vile –hutokea kutokana na sababu nyingine, hivyo sio lazima kuwa joto itokane tu na moto.

 

Watu wa moto (wenye kudai haya) wamesema kuwa: Inavyojulikana kuwa udongo na maji, vikichanganyika basi hapana budi kutokea joto ambalo hupelekea kupikika na kuchanganyika kwa viwili hivyo. Bila ya hivyo visingechanganyika, wala kuungana pamoja. Vile vile pindi unapotupa mbegu ardhini kiasi cha kutoifikia hewa wala jua haliifikii, huharibika mbegu hiyo. Basi lazima kutokea kitu cha kupika kuivisha kwanza katika umbo la mchanganyiko na ikitokea hivyo basi itakuwa ni chembe ya tabia ya kimoto. Kama haikutokea, basi umbo mchanganyiko halitapasha joto kwa tabia yake. Kama litapata joto, joto hilo likitoweka la mpito tu, na likipita joto hili la juu juu kitabaki sio cha joto chenyewe kwa tabia wala kwa namna yake nyingine kitakuwa baridi kabisa. Lakini baadhi ya vyakula na madawa kuna yaliyo ya joto kwa tabia yake hapo unapata kwamba joto la lake ni la asili ya moto. Vilevile, kama kwenye mwili kusingekuwa na chembe inayopasha joto, basi mwili ungefikia ukomo wa baridi.

 

Kwani tabia ikilazimu baridi, na kukakosekana kisaidizi au pingamizi, baridi lazima likomee upeo wake wa juu kabisa. Lau ingekuwa hivyo pasingetokea kuhisi baridi. Kwani baridi linalofika mwilini kama lina ukomo lingekuwa linafanana, na hakuna kuathiriwa kitu kutokana na mfano wake; yaani baridi haliwezi kuathiri baridi vile vile. Na kwa kuwa haliathiri, mtu asingehisi baridi. Na asingehisi baridi, asingepata maumivu yake. Na kama baridi litakuwa kiwango cha chini kuliko kilicho mwilini, basi kuathirika ndio zaidi. Kama kusingekuwako mwilini sehemu inayopasha moto, kimaumbile, basi mtu asingeathirika na baridi wala kupata maumivu kwa baridi.

 

Wanasema: Na dalili zenu hizo kusema kweli zinabatilisha yale wayasemayo kwamba: Chembe za kimoto husalia katika mchanganyiko wa maumbo kama zilivyo, na tabia yake ya kimoto, na sisi hatusemi hivyo bali twasema: Sura yake ilivyo katika asili huharibika pale inapochanganyika.

 

Wengine wamesema: Kwa nini isifae kusemwa: Kwamba ardhi na maji na hewa inapochanganyika: lile joto livishalo, lipikalo: Ni joto la jua, na nyota, sayari zingine. Kisha mchanganyiko ule, unapotimia kuiva huwa tayari kupokea umbo la mchanganyiko kupitia ujoto. Iwe mimea, wanyama, au madini, kizuizi kiko wapi kuwa joto hilo linalopatikana katika maumbo mchanganyiko ni kwa sababu ya sifa maalumu na nguvu ambazo Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Anazileta wakati wa kuwepo huo mchanganyiko na sio kwa kuwepo chembe za asili ya moto?[3]

 

Hamna njia yoyote kuweza kubadilisha uwezekano huu kabisa. Na kundi la matabibu bora kabisa wamekiri hilo.

 

Ama maelezo ya mwili kuhisi baridi, tunajibu kuwa: hiyo inajulisha kwamba kwenye mwili kuna joto, na kupasha joto. Kwani nani anakana hilo? Lakini nini dalili kuwa kinachopasha moto ni moto tu?  Kwani japo wajua kwamba kila moto huchemsha, kadhalika kwenye kadhia hii hili haijumuishi, bali kinyume chake ni kweli kuwa, baadhi ya inayochemsha ni moto.

 

Ama kauli yenu, mlipoelezea kuharibika sura ya moto wa asili; matabibu wengi wana msimamo kuwa sura ya asili ya moto ni yenye kusalia. Na kusema kuwa inaharibika ni kauli batili. Amekiri ubatili wa kauli hiyo, wa matabibu waliokuja nyuma katika kitabu chake kiitwaho “Ash-Shifaa”[4]. Ametoa hoja kuwa asili ya vitu hubaki kwenye tabia yake ndani ya maumbo mchanganyiko.  

 

 

[1]Amesema Imaam Shaafi’y (Rahimahu Allaah): “Sijashiba kwa muda wa miaka kumi na sita, isipokuwa nilishiba mara moja na kutoa (kutapika); kwani kushiba kunaupa uzito mwili na mashaka moyo na kuondosha utambuzi na kuleta usingizi na humdhoofisha mtu na ‘ibaadah.” [Imepokewa na Ibn Abiy Haatim katika ‘Aadab Ash-Shaafi’iy’ (uk 106)]

 

[2] Imepokewa na Al-Bukhari 6452

[3] Alichokiamua Imaam Ibn Al-Qayyim Al-Jawziyyah (Rahimahu Allaah) katika masuala haya ni yale yale waliyothibitisha wanazuoni wa elimu ya Hadiyth; viumbe hai vyote vinashirikiana katika mahitaji yake ya nguvu. Kadhalika suala la kupumua ni mtiririko wa silsila iliyoratibiwa katika katika maingiliano  (تفاعلات)za kibaolojia ambayo inakamilika kwa kuvunja vunja chembechembe (particles) za viungo vya kiwiliwili kuwa Carbon Dioxide na maji na nguvu, na kwa kuwa hizi  (تفاعلات) zinatimia na kutokea kwenye chembechembe hai, kwa hali hiyo imeitwa:  عملية التنفس الخلوي  )Cellular respiration(  Hili linatimia kwa   الميتوكندريا   (Al-Miytokandariyaa), hii ni sawa na kituo cha uzalishaji wa nguvu katika chembechembe hai, ambapo ndipo panapotokea mwingiliano (تفاعلات) wa ‘Cellular respiration.’

 

Kimefungwa na vifungo viwili, ambazo kwa pamoja na kifungo cha Plasma chenyewe ambacho ni:  Kifuniko cha nje ambayo ni nyeupe sana chenye kupenyeza mwanga (أملس), nayo imefungwa na mada nyingi za kikemia. Kifuniko cha ndani.

[4] Ni kitabu cha Shaykh Ar-Raiys: Abiy ‘Aliy Al-Husayn bin ‘Abdillaah bin Siynaa; anachukuliwa kuwa ni mwanafalsafa mkubwa katika hekima, mantiki, mazingira, ana baadhi ya makosa ambayo Uislamu hauridhiki na mfano wao. Miongoni mwa mwandishi. Kwa hivyo ikaoneshwa kwake kwa kauli yake: “Muta-aakhiriykum.” Shaykh Al-Islaam Ibn Taymiyyah na mwanafunzi wake Ibn Qayyim Al-Jawziyyah (Rahimahuma-Allaah) wanamtoa kasoro nyingi kwa kupotoka kwake kuliko kukubwa, alifariki mwaka 428 Hijriyyah.

 

 

Share