Imaam Ibn 'Uthaymiyn: Mwanamke Kuvaa Dhahabu Katika Sherehe Na Mikusanyiko Ya Furaha

 

Mwanamke Kuvaa Dhahabu Katika Sherehe Na Mikusanyiko Ya Furaha

 

Imaam Ibn ‘Uthaymiyn (Rahimahu Allaah)

 

www.alhidaaya.com

 

SWALI:

 

Je inaruhusika kwangu kuvaa dhahabu katika sherehe na mikusanyiko ya furaha?

 

JIBU:

 

Anaruhusiwa mwanamke kuvaa dhahabu katika sherehe na mikusanyiko ya furaha madamu tu wanaume wasiokuwa mahaarim wake hawataona, na kwamba walioko naye ni wanawake tu au ni wanaume ambao ni mahaarim wake.

 

 

[Fataawaa Nuwr ‘Alad-Darb Swali Namba 5757, Uk 202, Mj 11]

 

 

 

Share