45-Zawadi Kwa Wanandoa: Baina Ya Wakwe Na Mke Wa Mtoto Wao

 

Zawadi Kwa Wanandoa

 

45-Baina Ya Wakwe Na Mke Wa Mtoto Wao

 

بين الحماة والكنّة

 

 

Uislamu umefaradhisha kuwepo kwa maisha mema na kutendeana vizuri katika muamala familia, na akajaalia misingi ndoa ni mapenzi na kuhurumiana. Hivyo basi hapana budi kuwasiliana na kuoneana huruma pamoja na wengine ndani ya familia, na haswa zaidi jamaa zake mume na jamaa zake mke.

 
 

Na ajitahidi sana mke kutokuufanya moyo wa mume wake kuwa mgumu sana kwa ndugu za mume wake, na kufanya mambo mabaya ili mume awachukie ndugu zake ni kumuasi Allaah na Mtume Wake (Swalla Allaahu 'alayhi wa sallam) . Kuvunja udugu ni jambo lenye kuchukiza na huondosha mahusiano ya ki-dugu, na vile vile huufanya moyo wa mtu kuwa ni mgumu na huvunja kabisa sababu za kuwasiliana. Wake zetu ni taa za njiani na ni nuru ya maisha na wala sio moto uunguzao au mwiba unaochoma. Ni juu ya wanandoa kusoma Kauli Yake Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) inayosema:

 

وقضى ربك ألا تعبدوا إلا إياه وبالوالدين إحسانا

 

“ …na Mola wako Amehukumu kuwa msimuabudu yoyote ila Yeye tu. Na (Ameagiza) kuwafanyia wema  (mkubwa) wazazi”. (Al-Israa: 23)

 
 

Furaha ya ndoa inapatikana na kukua na inaendeelea kukua kadri mke atakavyomsaidia mumewe juu ya wajibu wake na kudumisha mahusiano yake (mke) nae na ya wengineo.

 
 

Mwanamke ni msaidizi wa mwanamme katika kumsaidia kumtii Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)  na kuwafanyia wema, upole, na kuwanyenyekea wazazi, ndugu, wake na waume wa watoto wao.

 
 

Uislamu unatahadharisha katika ufanyaji dhulma na udikteta  na huu ni mlinganio katika kusimamisha amani ya kudumu baina yake mzazi wa kike au wa kiume na mke wa mtoto wao wa kiume (ambae ni kama mtoto wake wa kuzaa) na inabidi kuamiliana nao kwa upole na kwa ukarimu na hapo ndipo yatakaposimama mahaba na kutengemaa kwa familia.

 

 

 
Share