Khitmah Kutokufaa Na Madhara Yake
Muhammad Baawazir
KHITMA NI NINI?
Khitma kilugha ni kuihitimisha Qur-aan nzima; kuisoma Qur-aan kuanzia mwanzo wake sura namba moja yaani Suratul Faatiha (Alhamdu) hadi mwisho wake ambayo ni sura namba 114 yaani Suratun Naas (Qul A'udhu birabbin Naas).
Lakini imegeuzwa maana hiyo ya kilugha na kugeuka katika matumizi ya walioanzisha huo utaratibu wa kumsomea Maiti Qur-aan na kuita kisomo hicho cha kumsomea Maiti kuwa ni Khitma kwa sababu ndani yake kuna kuisoma Qur-aan yote. Hukusanyana watu pahala; kwenye nyumba ya marehemu, au ukumbi wa kukodiwa au msikitini na kugawana juzuu kila mmoja na husomwa hiyo Qur-aan kwa sauti na kila mmoja kwa utaratibu wake na bila hata kumalizika. Pia huchomwa ubani n.k. Na wasomao hutaraji thawabu ya kusoma kwao hiyo Qur-aan imfikie Maiti. Na mambo haya yalianza baada ya kupita vipindi kitukufu cha vizazi vitatu ambavyo Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alivisifu.
Baada ya taarifu hiyo, maswali yafuatayo yanamiminika;
1) Watu wanaposoma Khitma husoma Qur-aan na kusoma Qur-aan ni jambo zuri na la ibada, sasa kwa nini isifae kuisoma kwenye Khitma?
2) Je, thawabu ya kusoma Qur-aan inamfikia Maiti?
3) Je, hayo yalifanywa na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) au Makhalifa wake waongofu au hata Maswahaba zake watukufu?
4) Madhara gani yanapatikana kwa kumsomea Qur-aan maiti?
5) Na
Haya ni maswali ambayo nimeyakusanya kwa ufupi kutoka kwa ndugu zetu waliouliza. Na nitajaribu kulijibu moja baada ya jingine kwa kadiri nitakavyowafikishwa na Allah (Subhaanahu wa Ta'ala)
1- Je kusoma Qur-aan sio ibada na jambo zuri? Kwa nini isifae kusoma Qur-aan kwenye Khitma wakati Qur-aan ni du'aa?
Bila shaka taratibu zote za dini yetu zinatoka katika Qur-aan na Sunnah za kipenzi chetu Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). Na mipangilio yote ya kiibada na sheria kaishatufundisha yeye na katuwekea mipangilio
Kwa sababu hakuna popote pale kwa ushahidi sahihi panapothibitisha kusoma Qur-aan kwa Maiti, basi jambo
Pia usomaji huo unaosomwa katika Khitma ni wa kelele na vurugu, kila mmoja husoma ki-aina yake na kwa kelele na wengi hawajui hata hukmu za tajwid. Na ingawa wanadai kuwa wanasoma Qur-aan kisha husoma na dua, Ukweli kusoma Qur-aan ni jambo zuri tena Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) katika hadithi iliyopo kwenye Al Bukhaariy na imesimuliwa na Abu Musa Al Ash'ary (Radhiya Allaahu 'anhu) anasema " Mfano wa yule Muislam asomaye Qur-aan ni kama Utrujjah (tunda lenye harufu nzuri), harufu yake nzuri na ladha yake tamu. Na Muislam asiyesoma Qur-aan ni
Hadithi hii hata hivyo haikuja kwa kuwasomea Maiti Qur-aan bali ni kuisoma kila wakati na kuonyesha umuhimu wa kuisoma Qur-aan kwa waumini. Na Qur-aan hiyo hiyo ikisomwa nyakati nyingine huenda ikampatia msomaji dhambi badala ya thawabu! Mfano mtu akaisoma Qur-aan chooni, au akiisoma kwa kutaka kumlogea mtu n.k.
Na pia kuisoma kwa Maiti kwa sababu ni jambo la uzushi basi hupelekea katika madhambi na hata motoni kutokana na hadithi ya Mtume katika riwaya nyingine aliposema: "Kila bid'ah ni upotofu na kila upotofu ni motoni" (Mwenyeezi Mungu atuepushe na
Na Mwenyeezi Mungu Anasema: {{Na isomwapo Qur-aan, isikilizeni, nyamazeni ili mpate kurehemewa}} 7:204. Na kwenye Khitma kila mmoja husoma kivyake na juzuu yake kwa sauti na hakuna mwenye kusikiliza.
Na anasema tena Mwenyeezi Mungu katika kuonyesha kuwa Yeye haihataji kuombwa kwa zogo na vurugu kwani Anajua akitakacho mja bila kupiga kelele na mayowe; Anasema: {{Na mtaje Mola wako kwa UNYENYEKEVU na khofu BILA KUPIGA KELELE katika kauli...}} 7:205
Na wanasema kuwa wao wanamkumbuka Mola wao na kumuomba, hata
2- Je, thawabu ya kusoma Qur-aan humfikia Maiti?
Naye Imam An Nawawy katika kufafanua kitabu cha hadiyth cha Imam Muslim, kwenye hadiyth hiyo akasema: "Ama kusoma Qur-aan na kukusudia thawabu za kisomo chake kimwendee maiti , na kusali ili thawabu zake zimfikie na mfano wa haya, amesema Imam Shaafi'i na Jamhuur ya wanachuoni (yaani wanachuoni wengi) kwamba haya hayamfikii maiti"
Imam Shaafi'i alipoulizwa kuhusu hilo akajibu kuwa thawabu ya kisomo haimfikii maiti na akatolea dalili hoja yake kwa aya isemayo: {{Na kwamba mtu hatapata ila yale aliyoyafanya}} 53:39 Na pia akatoa ushahidi wa hadithi : (Anapokufa mwanaadam hukatika amali zake ila kwa mambo matatu...) Taz. kitabu chake maarufu Al Umm Juzuu ya 4, uk.46
Pia katika kitabu maarufu cha madhehebu ya Ki-Shaafi'i kiitwacho Al Minhaaj, katika ufafanuzi uliofanywa na Ibnu Nahwy ni kwamba : "Hazimfikii maiti katika madhehebu yetu thawabu za kisomo katika kauli mashuhuri"
Aliulizwa Sultaanul 'Ulamaa Sheikh Al 'Izz bin 'Abdis-Salaam, mwanachuoni mkubwa wa Misr katika zama zake
Katika kitabu cha Assananu wal Mubtadaatu uk.216 kuhusu kumsomea Maiti Qur-aan, anasema mwandishi "Na kisomo cha Khitma ambazo wanazozifanyia watu waliokufa na kukusanyika kwenye Khitma hizo kwa kisomo, na kutawanyiana Juzuu... kutoka katika Msahafu kisha wanaanza kisomo na kumaliza kwa pamoja kwa kitambo kidogo tu kisha hupeleka hidaya thawabu walizozisoma kwa Maiti, ni
Naye mwanachuoni mkubwa maarufu wa tafsiri ya Qur-aan, Imam Ibn Kathir katika tafsiri ya suratun Najm aya ya 39 ameeleza kutokufaa kusoma Qur-aan na kufika thawabu zake kwa maiti.
Ni wanachuoni wengi maarufu waliopinga jambo hilo na sitoweza kuwataja yote waliyoyasema bali nitawataja baadhi yao tu kama mwanafunzi mkubwa wa Imam Shafi, Al Muzany, Abu Ishaaq Ash Shirazy na wengine wengi.
3- Je, hayo yalifanywa na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) au Makhalifa wake waongofu au hata Maswahaba zake watukufu?
Hakuna ushahidi wowote wala hadiyth yoyote sahihi au hata dhaifu inayoonyesha kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). aliwahi kusoma Khitma au kuwaambia watu wakusanyane na wamsomee maiti wao Qur-aan. Zipo Hadithi dhaifu na ma'udhuu zinasema kuwa maiti asomewe
Hivyo basi, hakuna ushahidi popote pale kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) wala Makhalifa wake waongofu au hata Maswahaba kwamba walifanya Khitma.
Kuna baadhi ya watu wa Khitmah wanaodai kuwa wakati ule Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). alipokuwa akifiwa na watu wake au marafiki zake na maswahaba kwa ujumla; kuwa Qur-aan ilikuwa haijashuka yote na hivyo asingeweza kufanya Khitma. Dai la namna hii ni dai potofu kwa sababu nyingi. Baadhi yake ni kuwa; huko ni kumfanya Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). kuwa hakuwa na maarifa kamili ya dini hii, na kwamba kuna mambo muhimu ya dini yetu aliyoyaacha na hakutufikishia! (M wenyeezi Mungu atuepushe na dhana
Jibu lingine ni kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). alifiwa na binti yake Ummu Kulthuum katika mwaka wa sita, na hapo Qur-aan ilikuwa imeshuka taqriban yote; sasa kwanini Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) asimsomee huyo mwanawe mtukufu kama jambo hilo lina manufaa kwa maiti?
Na hata alipokufa yeye (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). vipenzi vyake
4- Madhara gani yanapatikana kwa kumsomea Qur-aan maiti?
Madhara makubwa
Mtume amekemea
Anasema katika hadith aliyopokea mama wa waumini, bibi 'Aishah (Radhiya Allaahu 'anha) : "Mwenye kuanzisha jambo katika dini yetu hii, ambalo halimo, hurejeshewa nalo (halikubaliki mbele ya Allah)" Al Bukhaariy 2697
Nyingine: " Mwenye kufanya jambo ambalo halimo katika dini (sheria) yetu, basi huwa linamrejelea mwenyewe" Muslim 1718
Nyingine tushaitaja huko mwanzo nayo: " Nawausieni Ucha Mungu na usikivu na utiifu hata kama akiwa kiongozi wenu ni mtumwa (katika riwaya nyingine mtumwa mhabashi), na hakika atakayeishi baada yangu ataona khitilafu (tofauti)nyingi, basi (mtakapoona hali hiyo ya uzushi na ghasia katika dini) shikamaneni na sunna (mwenendo) wangu na sunna (mwenendo) wa Makhalifa wangu waongofu, na mzibane kwa magego (mzikamate kisawasawa). Na tahadharini na uzushi, hakika kila uzushi ni bid'aa na kila bid'ah ni upotevu" Abu Dawud 4607 na Attirmidhy 2676 katika riwaya nyingine 'kila upotevu ni kwenye moto (wa jahannam)'
Nyingine: "...Uzuri wa maongezi ni maongezi ya Kitabu cha Allah, Na ubora wa uongofu ni uongofu ulioletwa na Muhammad, na uovu wa mambo ni uzushi, na kila uzushi ni upotofu" Muslim 425
Na Hadiyth ziko nyingi
Na pia hadiyth nyingine na maneno ya wanachuoni yanatuonyesha ni jinsi gani kuna umuhimu na ubora wa kukamatana na kushikamanana na SUNNAH za Mtume wetu mpenzi (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na kuwa kila tunavyokamata Sunnah au kuzihuisha (kuzifufua) ndipo ujira wetu na kheri zinavyoongezeka. Na kukamatana na Bid'ah kunakimbiza kheri baraka na kueneza ufisadi na maasi katika jamii. Na ni bora kutosheka na Sunnah chache kuliko kukamatana na bid'aa nyingi.
Mwisho tuangalie kipengele cha tano chenye kuuliza:
5- Na
Hadiyth maarufu
Imam An Nawawy anasema katika kitabu chake cha Al Adhkaar uk.150 hivi: "Wamekubaliana wanachuoni kwamba dua za kumwombea maiti zinawanufaisha na zinafika thawabu za dua hiyo. Na wametoa hoja na dalili ya kauli yake Allah aliposema: {{ Na waliokuja baada
"Na nyinginezo miongoni mwa aya mashuhuri zenye maana
Pia Maulamaa wanaonelea kuwa miongoni mwa sadaka ni kumfanyia maiti Umra au Hajj ikiwa alikuwa hajafanya kwa ushahidi huu: "Mwanamke wa kabila la Juhayna alimuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). : "Mama yangu alikuwa na nadhiri ya kufanya Haji je, naweza kumlipia (kumhijia)? Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). akamjibu :" Mhijie. Je, mama yako angekuwa na deni usingemlipia? Basi, deni la Mola wako ni bora zaidi kulilipa" Al Bukhaariy
Na vilevile wanaonelea kuwa mtu anaweza kumfungia maiti yake Swawm ya nadhiri au aliyokuwa anadaiwa hajailipa kwa ushahidi huu: "Alikuja mtu kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam). akamwambia: "Ee Mjumbe wa Allah! Mama yangu amefariki na alipaswa kufunga swaum ya mwezi mmoja (aliyokuwa akidaiwa) Je, naweza kumfungia? Mtume akajibu kwa kuitikia kisha akamwambia: " Deni la Allah linastahiki zaidi kulipwa" Al Bukhaariy
Wengine wanaonelea kuwa yafaa hata kumlipia zile Swawm za deni
Haya ni mambo ambayo ni bora kuyafanya na yana ushahidi sahihi na ndio bora waislam wakayafanyia kazi zaidi kwani ndio yenye manufaa kwa wenzetu waliotangulia.
Namalizia hapa kwa kuwanasihi ndugu zangu turejee katika njia sahihi na mafundisho sahihi ya mtukufu Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam), na tuyaache yenye mashaka na yenye kutusababishia madhara katika dini yetu.
Mwisho namwomba Allah Atuongoze wote sisi katika njia iliyonyooka na atusamehe tuliyoyafanya bila elimu au kwa kurithi wazee na Masheikh wetu, na Atujaalie ni wenye kusikiza maneno na kufuata yaliyo mema.
Wa Allaahu A'alam
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


