Mwezi Wa Rajab: Fadhila Zake Na Yaliyozuliwa Ndani Yake
Muhammad Baawazir
Anasema Allaah سبحانه وتعالى
(( إِنَّ عِدَّةَ الشُّهُورِ عِندَ اللّهِ اثْنَا عَشَرَ شَهْرًا فِي كِتَابِ اللّهِ يَوْمَ خَلَقَ السَّمَاوَات وَالأَرْضَ مِنْهَا أَرْبَعَةٌ حُرُمٌ ذَلِكَ الدِّينُ الْقَيِّمُ فَلاَ تَظْلِمُواْ فِيهِنَّ أَنفُسَكُمْ))
((Hakika idadi ya miezi kwa Allaah ni miezi kumi na mbili katika hukumu ya Allaah tangu Alipoumba mbingu na ardhi. Katika hiyo iko minne mitakatifu. Hiyo ndiyo Dini iliyo sawa. Basi msidhulumu nafsi zenu humo)) [At-Tawbah: 36]
عن أبي بكرة - رضي الله عنه - أن النبي صلى الله عليه وسلم خطب في حجة الوداع وقال في خطبته إن ((الزمان قد استدار كهيئة يوم خلق السماوات والأرض السنة اثنا عشر شهرا منها أربعة حرم ثلاث متواليات ذو القَعدة وذو الحجة والمحرم ورجب مضر الذي بين جمادى وشعبان )) رواه البخاري
Kutoka kwa Abu Bakrah رضي الله عنه kwamba Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alitoa Khutbah yake ya mwisho akasema: ((Wakati umemaliza mzunguko wake
Na Anasema Allaah:
((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُواْ لاَ تُحِلُّواْ شَعَآئِرَ اللّهِ وَلاَ الشَّهْرَ الْحَرَام ))
((Enyi mlioamini! Msivunje hishima ya alama ya Dini ya Allaah wala mwezi mtakatifu)) [Al-Maaidah: 2]
Hapana shaka kutokana na Aayah hizo kwamba miezi hii minne mitukufu hutakiwa kutukuzwa inavyopaswa, kwa kutokufanya maasi na kudhulumiana, kwani malipo ya kufanya madhambi katika miezi hii mitukufu huwa ni makubwa zaidi. Katika kuiheshimu pia ni kumcha Allaah zaidi kwa kila aina ya ibada. Lakini sio kwa kuchagua siku maalumu ambazo watu wametenga kwa ajili ya kusherehekea na kumshukuru Allaah kutokana na kuaminika utukufu wa siku hizo au matukio yake ya kihistoria.
Mifano ya mambo yanayotendeka katika mwezi huu ambayo hayana uthibitisho kutoka katika Qur-aan wala Sunnah Sahihi:
· Kuitukuza siku inayosemwa ni ya Mi’iraaj au Israa na Mi’iraaj (ambayo inadaiwa na wengi kuwa ilikuwa katika mwezi huu wa Rajab, na kudaiwa ni tarehe 27) kwa kufunga hasa siku hii pekee.
· Baadhi ya watu wameanzisha Swalah ambayo wameiita Swalaat Ar-Raghaib, ambayo huswaliwa mwanzoni mwa mwezi huu. Hii ni kama ile hali ya mwezi wa Sha'abaan na haswa katikati yake ambayo watu wamezusha jina liitwalo Laylatul baraat (wakisema ni usiku wa ahadi na kusamehewa waliokufa au ni usiku wa kuwekwa mbali na madhambi) ambapo watu hufanya ni usiku wa ibada na kuswali sana na kufunga mchana wake.
· Watu wametunga du'aa na aina ya Istighfaar na dhikr mbali mbali kuwa ni maalumu zisomwe katika mwezi huu wa Rajab.
· Kuzuru makaburi.
· Watu kujumuika na kufanya mihadhara na kupeana mawaidha ya kuelezana historia ya tukio la Israa na Mi'iraaj.
Hizi ni sherehe na mipangilio ya ibada ambayo hayamo katika sheria katu, na wala hazijathibiti katika ushahidi sahihi sehemu yoyote katika vyanzo vya kutegemewa. Ni mambo ya uzushi ambayo baaadhi ya watu wameyazusha kwa ajili ya kuzitukuza siku hizo kutokana na kudhani kufanya hivyo kutawapatia ujira na kuwaongezea daraja
Ukifanya utafiti na kupitia katika maandiko yenye kutegemewa, utakuta hakuna uthibitisho wa kusherehekea na kufanya ibada zozote maalum katika siku hiyo na usiku huo. Pia hakuna ushahidi sahihi wa kufunga Swawm katika siku hiyo ya tarehe 27 ya mwezi wa Rajab.
((Allaah Anawatazama viumbe wake katika usiku wa kumi na tano wa Sha'abaan na kisha huwasamehe ila wale washirikina au wale wenye kuwa na Uadui))
Hakuna ushahidi na ukweli halisi wa kuwa usiku huo wa safari tukufu ya Mtume wetu صلى الله عليه وآله وسلم ya Israa na Mi'iraaj, kuwa ulikuwa ni katika siku hii ya tarehe 27 ya Rajab, na hata kama ikisemwa kuwa ilikuwa ni siku hiyo na wasio na ushahidi, bado hakuna mafundisho yoyote yenye kutueleza kuwa tunapaswa kufunga katika siku hii.
Na
Ama ya kukusanyana katika siku hiyo ya tarehe 27 Rajab, kwa ajili ya kupeana mawaidha na kuelezana historia ya tukio hilo, ni bora liepukwe na ni vizuri kuwahimiza watu kuhudhuria madarsa misikitini na mihadhara ili waweze kuyajua hayo na mengi mengine ambayo ni muhimu zaidi katika dini yao. Kuwepo kwa minasabaat
Hata kwenye baadhi ya kalenda kumewekwa siku hizo
Ikiwa inamwekea Muislam sheria na kudai ni za kigaidi, na katiba za kumnyima haki zake na kumnyanyasa na kubana uhuru wake wa kuabudu na kutangaza dini ya Allaah, je, inakutakia kheri gani Muislam kwa kukupa siku ya ziada kwa kusherehekea mazazi ya Mtume? Ikiwa ndio hiyo hiyo iliyowapiga virungu, risasi na kuua Waislam na kuwadhalilisha waumini msikitini bila kuwastahi kinamama, leo itakuwa inakuthamini vipi wewe? Suala ni kuwafumba Waislam macho kwa yasiyo ya msingi na kuwashughulisha nayo ili wabaki wamelala na wasidai haki zao au kuzipigania. Na lil-asaf shadiyd, (sikitiko kubwa) Waislam wengi wametumbukia katika hila hizo ndogo
Amiyrul-Muuminiyn ‘Umar رضي الله عنه alikuwa akikataza watu kufunga mwezi huu kwa sababu ilihusiana na kushabihiana na Ujahiliya.
Inaelezwa Kwamba Kharashah ibn al-Harr alisema: "Nimemuona ‘Umar akiwachapa mikono wale waliokuwa wakifunga Rajab walipokuwa wanafikia chakula chao na alikuwa akisema, huu ni mwezi walioufanya mtukufu katika Ujahiliya" [al-Irwaa’, 957; Shaykh Al-Albaaniy kasema ni Sahihi].
Imaam Ibnul Qayyim رحمه الله amesema katika kitabu chake cha Zaadul Ma'ad: ''Hakuna ushahidi ulio wazi wa kuwa ni mwezi au tarehe gani tukio hili lilitokea. Kuna taarifa nyingi kuhusiana na jambo hili (kuwa lilifanyika mwezi huu wa Rajab) lakini hakuna hata moja katika taarifa hizo yenye uamuzi kamili na sahihi. Na hakuna ibada zozote maalum zenye kufungamana nayo.''
Kwa ujumla siku zote za Muislam ni nzuri na bora kwa kuwa Allaah سبحانه وتعالى Huwa Anashuka kila usiku katika fungu la tatu la usiku
عن أبي هريرة رضي الله عنه أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: ((ينزل ربنا تبارك وتعالى كل ليلة إلى السماء الدنيا حين يبقى ثلث الليل الآخر فيقول: من يدعوني فأستجيب له؟ من يسألني فأعطيه؟ من يستغفرني فأغفر له )) البخاري
Imetoka kwa Abu Hurayrah رضي الله عنه kwamba Mtume صلى الله عليه وسلم amesema: ((Allaah سبحانه وتعالى Huteremka kila siku katika mbingu ya dunia (mbingu ya kwanza) inapobakia thuluthi ya mwisho ya usiku na Husema: Nani ananiomba Nimtakabalie? Nani ana shida Nimtekelezee? Nani ananiomba maghfira Nimghufurie? )) [Al-Bukhaariy[
Kuna masiku mengi yenye fadhila
((Hakuna matendo mazuri yafanywayo katika masiku mengine yakawa bora kuliko yafanywayo katika masiku haya (ya mwanzo wa mwezi wa Dhul-Hijjah)''. Kisha baadhi ya Maswahaba wakamuuliza: ''Kuliko hata Jihaad?'' Akawajibu: Kuliko hata Jihaad, isipokuwa tendo la mtu atakayefanya kwa kujiingiza hatarini yeye na
Masiku kumi ya mwisho ya mwezi wa Ramadhaan ni matukufu zaidi kuliko michana kumi ya mwezi wa Dhul-Hijjah na masiku kumi ya mwezi wa Dhul-Hijjah ni matukufu zaidi kuliko michana ya mwezi wa Ramadhaan. Haya ni maoni yenye nguvu ya Maulamaa. Ama siku iliyo bora kuliko zote basi ni siku ya 'Arafah, kwani imesimuliwa kuwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم alisema:
((Hakuna siku iliyo na fadhila kuliko zote mbele ya Allah
Mifano hiyo ni kuonyesha kuwa masiku yaliyotajwa hapo juu ni bora kwa Muislam na yaliyo munasibu kwa kumwabudu Allaah سبحانه وتعالى. Na Allaah سبحانه وتعالى Kazipa ubora baadhi ya nyakati kuliko zingine kwa kumpa tu mtu fursa ya kufanya zaidi matendo mema kwa kadiri awezavyo, na matendo hayo ni muhimu kwa Muislam kwa maisha yake ya hapa duniani na akhera. Na ukitazama utakuta yote yamewekwa wazi na Mtume صلى الله عليه وآله وسلم na jinsi ya kutekeleza ibada katika masiku au nyakati hizo. Ama zile ambazo hazijatajwa na kuwekwa wazi basi ni bora na vizuri tuziache na kujiepusha na kufanya matendo ndani yake ambayo hatukufundishwa. Nako kutakuwa bora katika dini yetu na hadhi yetu,
عَنْ أَبِي عَبْدِ اللَّهِ النُّعْمَانِ بْنِ بَشِيرٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُمَا قَالَ: سَمِعْتُ رَسُولَ اللَّهِ صلى الله عليه وآله وسلم يَقُولُ: (... فَمَنْ اتَّقَى الشُّبُهَاتِ فَقَدْ اسْتَبْرَأَ لِدِينِهِ وَعِرْضِهِ ... ) رَوَاهُ الْبُخَارِيُّ
((...atakayekaa mbali na utata, basi atakuwa ameilinda (ameitakasa) Dini yake na heshima yake...)) [Al-Bukhaariy]
Wa Allaahu A'alam
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha

DINI HAIENDI KWA RAI YA
DINI HAIENDI KWA RAI YA MTU
Assalaam Aleikum Ndugu Mukhtar Mahmoud,
Amma baada ya salaam, ningependa kuchukua fursa hii kukuonyesha hatari ya hayo unayoitakidi.
Ndugu yangu katika imaan, tunapo aacha mamabo tuliyo amrishwa tuyatekeleze, imma kwa kutokujuwa au kupuuzia, mfano kitendo cha kumswalia Mtume Muhammad ( Rehma za Allaah na amani ziwe juu yake) kikamilifu hata kama ni kimaandishi na vile vile katika kutoa salaamu. Ninge kushauri utembelee tovuti hii ya Alhidaaya kwenye link hii, illi kufahamu umuhimu wa salaamu http://www.alhidaaya.com/sw/nasiha_kiislamu
Ndugu Mukhtar hii dini imeshakamilika, hakuna ibaada itakayo tukaribisha kwa Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) isipokuwa Mtume Muhammad ( Rehma za Allaah na amani ziwe juu yake) ameshatufunza.
Allah (Subhaanahu Wa Ta'ala) Anasema:-
Leo nimekukamiliishieni Dini yenu, na nimekutimizieni neema yangu, na nimekupendeleeni UISLAMU uwe ndiyo Dini. Al-Maidah:03
Au hao wana miungu ya kishirikina walio watungia dini asiyo itolea idhini Mwenyezi Mungu? As-Shuura:21
Imepokelewa Kutoka Mama wa waumini Aisha (Radhi za Allaah ziwe juu yake) ya kwamba Mtume Muhammad ( Rehma za Allaah na amani ziwe juu yake) amesema Yeyote atakaye tenda jambo (Ibada) ambalo haliko katika dini yetu, basi atarudishiwa mwenyewe (Haitokubaliwa). Bukhari.
Haikuwa kwa Mayahudi na Manaswara dini kwenda kombo illa baada ya kwisha kupata uongofu kutoka kwa Mitume wao, ispokuwa pale walipo acha yale walio funzwa na kuanza kuingiza ya kwao. Vizazi vilivyo kuja baadae wakashindwa kubainisha ipi ni ibada halisi na ipi ni nyongeza.
Nikikutolea mfano hai, leo mmoja wetu akifiwa, anapata msiba mara mbili, wakumkosa mtu wake na kugharimia wanaomhani, wakati Mtume Muhammad ( Rehma za Allaah na amani ziwe juu yake) amesema nyumba iliofiwa isiwashwe moto.!!!!!!!!!
Ndugu Mukhtar hii dini si tuonavyo sisi, bali ni ilivyo pokelewa kutoka kwa Mtume Muhammad ( Rehma za Allaah na amani ziwe juu yake) hadi kutufikia sisi.
Tuna njia nyingi sana za kufanya Ibada zisizokuwa na utata, kwa nini tunalazimisha mambo ambayo ya kuzushwa.
Umesema " itakuwa si vibaya kuitukuza siku hiyo (Nisfu Shaaban) kwani itakuwa hatujajiwekea siku maalum za ibada," Kama hii si siku maalum, ni ipi unayo ikusudia hapa?
Amma kuhusu maulidi tafadhali bonyeza link hii hapa chini,
http://www.alhidaaya.com/sw/node/3782
Nduguyo ktk Imaan
Abu Haashim
A.laikum,
A.laikum, alhamdulillah,article yako iliopo hapo juu nimeweza kuifahamu. Na mie kwa upande wangu ninavohisi ni kwamba siku alizozitaja bwana wetu Muhammad S.A.W kwamba ni tukufu na tuzitumie kwa ajili ya kuchuma thawabu na kupata radhi za allah, ni kweli kwamba siku hizo ni tukufu. lakini kwa upande mwengine, hata kama mtume hajatuambia kuitukuza Nisfu Shaabaan, haina ubaya katika kuitukuza kwani hatukufuru na pia kama tutakuwa tunafanya ibada kama swala na kufunga kila siku, itakuwa si vibaya kuitukuza siku hiyo, kwani itakuwa hatujajiwekea siku maalum za ibada, na tukitizama mambo yanayofanyika katika siku ya nisfu shaabaan ni mazuri kama kuomba dua sana na kuzuru makaburi, tunapata thawabu kwasababu tunafanya kwa ajili ya allah kwa kutarajia malipo. Na kuhusu maulidi, kama mtu atakuwa anaipa maulidi hadhi kubwa kuliko swala na nguzo za islaam, basi huyo yuko katika makosa, lakini kama huyo mtu anaehudhuria maulidi na kashikamana vizuri na nguzo za uislaam basi hafanyi jambo baya, anajua mipaka ya kila ibada, na pia maulid inaingia katika kundi la bid'ah HASSAN.
Assalam alaykum warahmatu
Assalam alaykum warahmatu llahi wabarakatuh
Shukrani zote zinamstahiki Allah Subhhana wataala na sala na salam zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad Swala llahu alayji wasalam na sahaba wote wema.
Mimi naona inafaa kwa mashekhe kuwa na kauli moja mana sisi ambao tunasoma kupitia kwenye source za dini au hata madarsa tunapewa vitu tofauti ambavyo vinachanganya. wengine wanahimiza nyiradi za mwezi huu wa Rajabu na wengine wanakataza.
Kwa kila mtu ambae anaambiwa kuwa kuna dua au nyiradi za kukufutia makosa yako naamini kila mtu antafuata.
mimi nimeelewa vizuri mada yako, ila hayo ndio maoni yangu
Jazakum llahi kheyri
Assalam Alaykum, Ahsante
Assalam Alaykum,
Ahsante sana kwa makala haya yanayoonyesha na kubainisha mambo mengi yanayofanywa na Waislamu kumbe hata hayatajwa katika dini. Its a great source of learning.
Jazakallahu kheyr