04-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Asitamani Mauti

 
Asitamani Mauti
 
Kadiri mgonjwa atakavyohisi uchungu katika maradhi yake haimpasi yeye au hata jamaa zake kutamani yamfike mauti.
 
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, ‘Asitamani mmoja wenu mauti kwa dhara au ugonjwa uliomsibu, ikiwa hapana budi kufanya hivyo basi na aombe dua hii, ‘Ee, Mola wangu nihuishe maadamu maisha yangu yatakuwa na kheri nami, na nifishe ikiwa kufa kwangu itakuwa ni kheri kwangu (kuliko kuishi kwangu)” (Bukhari na Muslim)
 
Ikiwa mja ni mwema basi ziada ya umri wake itakuwa ni kuongeza wema wake juu ya wema aliokuwa nao, na ikiwa ni mja muovu basi yale maumivu ayapatayo katika ugonjwa wake humuondolea madhambi yake na hiyo vile vile ni fursa yake ya kutubia na kurejea katika Istighfar kwa yale aliyepetuka mipaka katika haki ya Allah (Subhaanahu wa Ta'ala).
 
Amesema tena Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) “ Mbora katika watu ni yule mwenye umri mrefu na matendo yake yakawa mazuri” (Tirmidhi na Ahmad)
Share