10-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Usia kwa theluthi ya mali au chini ya hapo

 
Usia kwa theluthi ya mali au chini ya hapo:
 
 
Inajuzu kuusia mali theluthi moja tu, haifai kuzidisha zaidi ya hapo, ni vizuri zaidi ikawa ni chini ya theluthi.
 
Sa’ad bin Waqas (Radhiya Allaahu 'anhu) amesema, ‘Nilikuwa pamoja na Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) katika hijja ya kuaga (Hijjatul wadaa) nikaugua maradhi ambayo yalinikurubisha na mauti, Mtume akaja kunitembelea, nikamwambia, ‘Ee, Mtume mimi nina mali nyingi na sina mrithi zaidi ya binti yangu mmoja, je, niusie kwa theluthi mali yangu? Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akasema, “Hapana” nikasema, ‘kwa sehemu ya mali’? Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akasema, “Hapana” nikasema, “ Theluthi ya mali yangu?” Mtume akasema, “theluthi, theluthi ni nyingi, ee, Sa’ad kuwaacha warithi wako mali nyingi, matajiri ni bora kwako kuliko kuwaacha kama mzigo wakiomba omba watu.” Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akaendelea kusema, “Ee, Sa’ad hutotoa utakachokitoa kwa kutamani ujira wa Mwenyezi Mungu ila Mwenyezi Mungu atakulipa kwa hilo, kiasi hata tonge unalompa mkeo.” (Bukhari na Muslim)
 
Share