11-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kuacha kufanya maovu (madhara) katika kuusia

 
Kuacha kufanya maovu (madhara) katika kuusia:
 
 
 Katika mambo ambayo hayatakiwi kufanyika wakati unapousia ni kuwausia baadhi ya warithi kwa yasiyokuwa haki zao. Au kutoa usia kuwa mmoja katika warithi wake asirithi nayo ni haramu na kinyume na hukumu na sheria ya Allah (Subhaanahu wa Ta'ala).
 
Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) amesema, “…Baada ya kutoa vilivyousiwa au kulipa deni, pasipo kuleta dhara…” (4:12)
 
Imethibiti kutoka kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) kuwa amesema, “Hakuna dhara au kudhuriana, atakayefanya madhara basi Mwenyezi Mungu atamdhuru, na atakayefanya ugumu basi Mwenyezi Mungu atamfanyia ugumu.”
Share