18-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kulipa Deni kwa mali ya Maiti

 
Kulipa Deni kwa mali ya Maiti:
 
 
Ni juu ya jamaa za maiti kumlipia maiti madeni anayodaiwa katika mali ya maiti, kama atakuwa ameacha mali hata ikibidi kutolewa mali yote isibakie kitu baada ya kutolewa madeni.
 
Kutoka kwa Sa’ad bin Al-Atwal (Radhiya Allaahu 'anhu) alisema kuwa nduguye alifariki akaacha dirham mia tatu, hali kadhalika alikuwa ameacha watoto. Sa’ad akasema, ‘ Nilitaka mali ile iwafae wale watoto wake yule aliyefariki, Sa’ad akasema, ‘Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akaniambia, “hakika ya nduguyo ni mfungwa wa deni analodaiwa, mlipie deni hilo.” Nikajibu, ‘Ee, Mtume wa Allah, nimeshamlipia deni lake ila ilbaki Dinari mbili ambazo nimempa mkewe na hana bayina kwake, Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akasema, “mpe hakika yeye ni mwenye haki nazo.” (Ibn Majah, Ahmad na wengineo)
Share