20-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Walii kumlipia deni maiti

Walii kumlipia deni maiti:
 
 
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alipokuwa analetewa mtu aliyekufa mwenye madeni huuliza, “Je, ameacha wa kumlipia deni lake?” akiambiwa kuwa ameacha wa kumlipia humswalia lakini kama hajaacha huwaambia sahaba zake, “Mswalieni sahibu yenu.” Mwenyezi Mungu alipomfungulia yeye na Waislamu nchi nyingi zikawa katika himaya ya Uislamu akawa anasema, “Mimi ni wa mwanzo kuliko waumini wengine katika jambo hilo, hivyo atakayekufa na akaacha deni basi ni juu yangu mimi kulilipa deni hilo, na atakayeacha mali basi mali hiyo ni ya warithi wake.” (Bukhari na Muslim) 
Share