22-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kilio chenye kukubaliwa kisheria

Kilio chenye kukubaliwa kisheria:
 
Hapana shaka kuwa msiba unapomfika mtu wa kufiliwa kwa mpenzi wake, jamaa zake na ndugu wa karibu unakuwa ni mkubwa kwa mtu na unaweza kumchanganya mtu na hilo ni jambo la kawaida, dini yetu tukufu haiendi kinyume na hisia za kimaumbile za mwanadamu lakini pamoja na hivyo huzielekeza hisia hizo katika sehemu itakiwayo bila ya kumchukiza na kumkasirisha Allah (Subhaanahu wa Ta'ala).
Katika sahihi mbili tunasoma kadhalika, ‘Kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alipofiwa na mwanawe Ibrahim alilengwa na machozi kisha akasema, “Hakika jicho hutoa machozi, na moyo unahuzunika, hatusemi ila kile chenye kumridhisha Allah (Subhaanahu wa Ta'ala) na hakika kuachana nawe Ibrahim tunahuzunika.”
 
Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alijiwa na baadhi ya wajukuu zake akiwa katika hali ya kifo, akalia akaulizwa, ‘Ni nini Ee Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam)? mtume akajibu, “hii ni huruma na Mwenyezi Mungu huwahurumia waja wake wenye kuwahurumia wenzao.” (Bukhari na Muslim)
Ama hadithi nyingine katika hadithi kama hizi, Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alisema, “ Si katika sisi anayechana nguo, kujipiga mashavu na akapiga kelele za Jaahiliya.” (Bukhari na Muslim) Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) ametuelezea kuwa mambo haya ni katika mambo ya wakati wa ushenzi (Jaahiliya) na ni mambo ya kikafiri.
 
Share