32-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Swala ya Jeneza

 
Swala ya Jeneza:
 
 
Suala hili la kuswaliwa maiti ni katika jambo kubwa ambalo maiti ananufaika nalo. Hivyo basi katika wale wanaopenda maiti wao wafaidike na hili ni vizuri wakaona kuwa idadi ya wanaomswalia maiti ni wengi tena wengi wao ni wale wema Mukhliswiin miongoni mwao. Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, “ Hakuwa maiti atakayeswaliwa na watu wanaofika mia moja na wote wakamuombea isipokuwa Mwenyezi Mungu atakubali maombezi yao.” (Muslim). Hali kadhalika katika hadithi nyingine tena Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, “Hakuwa Muislamu aliyekufa na watu wakasimama katika jeneza lake wakafikia arobaini hawamshirikishi Mwenyezi Mungu na chochote ila Mwenyezi Mungu atakubali maombezi yao.” (Muslim)
Share