36-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Muda unaokatazwa kuswalia jeneza na kuzika

 

Muda unaokatazwa kuswalia jeneza na kuzika:

 

Kutoka kwa Uqbah bin ‘Amir (Radhiya Allaahu 'anhu) amesema, ‘Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) ametukataza kuswalia na kuzika maiti katika nyakati tatu; pindi linapochomoza jua hadi linapotulia juu, pindi jua linapokuwa katikati hadi linapopinda, pindi jua linapoanza kuzama hadi linapokuwa limezama kabisa.’ (Muslim)

Nyakati zenyewe ni hizi: linapochomoza hadi baada yake kama dakika ishirini hivi hadi nusu saa, kabla ya Swala ya Adhuhuri kwa dakika ishirini hadi inapoadhiniwa adhuhuri, kabla ya Maghrib hadi linapozama kabisa jua.

Share