35-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kulipeleka upesi Jeneza

 

 

Kulipeleka upesi Jeneza:

 

 

Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) amesema, “Lipelekeni upesi jeneza likiwa ni la mtu mwema basi mtakuwa mnamuwahisha kwenye kheri yenyewe na likiwa kinyume na hivyo basi mnaondosha shari kwenye mabega yenu.” (Bukhari na Muslim)

Katika hadithi nyingine amesema, “Litakapowekwa jeneza na watu wakaweka katika mabega yao, basi likiwa ni la mtu mwema litasema, “Nipelekeni, likiwa la mtu asiye mwema litasema, “Ole wangu wananipeleka wapi?! Kila kitu kinasikia sauti ile isipokuwa mwana adamu tu na lau akilisikia basi atapata mshtuko mkubwa unaoweza kumuangusha ….(saaka).” (Bukhari)

 

Share