44-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Je, wafiwa huwatengenezea wahani chakula?

 

 

Je, wafiwa huwatengenezea wahani chakula?

 

 

Haifai kwa wafiwa kutengeneza chakula kwa wahani, lakini kinyume chake ndio sahihi wao ndio wenye haja haswa ya kutengenezewa chakula kwa msiba waliokuwa nao, huzuni ambayo inawafanya kukosa hamu ya kula, hivyo basi ni katika Sunna kwa jamaa wa karibu wa maiti (wasio kuwa wafiwa wa daraja la mwanzo) pamoja na majirani zao kuwatengenezea wafiwa chakula kitakachowatosheleza.

Share