52-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kuacha huru mtumwa, kutoa sadaka na kuhiji humnufaisha Muislamu

 

 

Kuacha huru mtumwa, kutoa sadaka na kuhiji humnufaisha Muislamu:

 

 

Abu Daud na wengineo wamepokea kuwa, “ ‘Al-Aas bin Wail As-sahami aliusia waachwe huru watumwa mia moja, mwanawe Hisham akawaacha huru watumwa hamsini tu. Mwanawe mwingine aitwae Amruu akataka kuwaacha wale watumwa wengine hamsini waliobakia, akaenda kwanza kumuuliza Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam). alipomfikia akamuuliza, ‘Ewe Mtume wa Allah, hakika baba yangu ameusia waachwe huru watumwa mia moja, lakini ndugu yangu Hisham amewaacha watumwa hamsini tu, hivyo wamebaki hamsini. Je, niwaache huru? Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akajibu, “lau baba yenu angelikuwa Muislamu na mkaacha huru watumwa au mkamtolea sadaka au mngelimhijia basi angenufaika na hayo na malipo yake yangemfikia.”

 

Share