53-Dalili Za Kheri Katika Mambo Yamfaayo Maiti: Kumhijia asiyehiji

 

 

Kumhijia asiyehiji:

 

 

Imepokewa na Bukhari kuwa: mwanamke kutoka kabila la Juhayna alikwenda kwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam), akamuuliza, ‘Mama yangu aliweka nadhiri kuwa atahiji lakini hakuhiji hadi alipofariki, je, nimuhijie? Mtume akamjibu, “Ndio, mhijie, je, huoni kuwa kama mama yako angekuwa anadaiwa ungelipia deni lake? Tekeleza deni la Mwenyezi Mungu na Yeye ndiye Mwenye haki ya kulipwa deni lake.”

Katika Sahihi Muslim inasmuliwa kuwa mwanamke kutoka kabila la Khath’am alisema, ‘Baba yangu ni mzee sana na ana faradhi ya Hijja ambayo hakuitekeleza naye hawezi kukaa juu ya mgongo wa mnyama. Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akamjibu, “Mhijie.”

Katika hadithi nyingine sahihi iliyokuwa mashuhuri, ‘kuwa Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) alimsikia mtu akisema, ‘Labaika Allahumma kwa Shubruma, Mtume akamwambia mtu yule, ‘Je, huyo Shubruma ni nani? Yule mtu akajibu, ‘Ni ndugu au jamaa yangu wa karibu.’ Mtume (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa Sallam) akamuuliza, ‘Je, wewe mwenyewe umehiji.? Yule mtu akajibu, ‘hapana.’ Hapo Mtume akasema, “Jihijie mwenyewe kwanza kisha muhijie Shubrama.”

 

 

Share