04-Uswuul Al-Fiqhi: Sura Ya Kwanza- Taratibu Za Uchunguzi Na Elimu Ndani Ya Fikhi Ya Kiislamu.

 

 

Maana:

 

Sayansi ya chanzo cha utaratibu wa Fiqhi ya Kiislamu Uswuul al-Fiqh imetafsiriwa kama ni mkusanyiko ulio pekee na maana maalum, wa uthibiti wa kisheria na ushahidi ambao, utakaposomwa kwa makini, utapelekea aidha kwenye elimu mahsusi ya uamuzi wa Shari’ah ama kwa uchache kwenye dhana yenye kueleweka inayohusisha hayo hayo. Utaratibu ambao kwa thibati hizo umechukuliwa na hali ya mthibitshaji.[1]

 

Kiini cha Hoja:

 

Kama ambavyo ni kiini cha hoja. Sayansi hii, pamoja na thibati zilizomo ndani ya vyanzo vya maandiko ya Shari’ah. Huziangalia kupitia mtazamo wa namna yake kwa maana ya Ijtihaad. Hukumu za kisheria zinatolewa kutokana na kipengele kimoja baada ya kimoja. Ingawa baadaye, kwenye kesi ambapo maandiko inatokea kwa pamoja kukhalifiana. Hiari ya uchaguzi imewekwa bayana[2].

 

Manufaa:

 

Sayansi ya Uswuul al-Fiqh inafanya uwezekano wa kuwa na elimu ya maamuzi ya Shariah kama ni somo, kwa upande wa wale wenye sifa za kufanya Ijtihaad na ambao wamefaulu masharti yake ya thibati za kisheria zilizotolewa na Mtoaji wa Sheria (Allaah).

 

Faida zinazopatikana kutokana na sayansi hii kwa wale wasiofaa kufanya Ijtihaad ni kwamba; kupitia masomo yao ya skuli bora za dhana za kisheria madhaahib za mujtahiduun (wale ambao wanatumia Ijtihaad) na hoja chini ya maamuzi yao. Wanafunzi wa somo la utaratibu wa uchunguzi ndani ya Fiqhi ya Kiislamu hawawezi kuelewa matawi tofauti ya dhana, kuzichambua na kuchagua kutoka miongoni mwa tafsiri na kufanya uchaguzi (wa hoja iliyo bora), na kuthibitisha mijadala ya kisheria kwa mnasaba wa kanuni zilizotolewa na mujtahiduun walio bora.

 



[1] Angalia Fakhrud-Diyn ar-Raazi; Al Mahswuul Fi ‘ilm Uswuul al-Fiqh, iliyohakikiwa na Dkt. Twaah Jaabir al-‘Alwaaniy; Riyaadh; Imamu wa Chuo Kikuu cha Kiislamu cha Ibn Sa’ud, toleo la mwanzo; 1399/1979; sehemu ya 1, uk. 94.

[2] Angalia maelezo juu ya Uswuul al-Fiqh yaliyoanzishwa na Maprofesa wa kitivo cha Sheria, Chuo Kikuu cha Al-Azhar, mwaka wa masomo 1382/1963 uk.22

Share