15-Uswuul Al-Fiqhi: Fuqahaa Miongoni Mwa Swahaabah Na Taabi’uun

 

Fuqahaa Miongoni Mwa Swahaabah Na Taabi’uun

 

 

 

Kipindi hichi kinaaminika kuwa kimeanza kwa kupita kipindi kilichoitangulia, mwaka 40 Hijriyyah, pale kipindi cha Maswahaba wakuu walioongoka vyema kilipomalizika. Hivyo, ikaanza tarehe mpya, ile ya Fuqaaha kutoka miongoni mwa Swahaabah na wazee wa Taabi’uun. Sheria katika wakati huu bado sana ilikuwa kama wakati uliopita, kwani vyanzo vya sheria hiyo, yaani Qur-aan, Sunnah, IIjmaa’ na Qiyaas, vilibaki kama vilivyo. Hata hivyo, sheria kwa wakati huo ilitofautiana kwenye nyanja nyingi kulingana na ule uliopita kabla.

 

Miongoni mwa mabadiliko yenye maana yalikuwa yafuatayo:

 

1.       Wanachuoni wamekuwa wanapendelea zaidi kuchimbua kupita kiasi maana za maandiko kwa uwazi.

 

2.       Njia zao za kujadili Sunnah zilipatwa na mabadiliko makubwa. Hakika, tofauti hii ni tokeo la tofauti za kisiasa zenye kushikamana na kuibuka kwa madhehebu tofauti na walio na fitna thaabit, kama vile Shi’ah na Khawaarij, ambao nia zao kwa Sunnah zilikuwa ni tofauti. Hao Shi’ah walikaidi kukubali Hadiyth zilizokuwa hazijapokelewa na wafuasi wao wenyewe; na Khawaarij walikaidi kukubali Hadiyth kama, popote kwenye mfululizo wa wapokezi wa Hadiyth hakuna hata upokezi mmoja[1]. Khawaarij pia walizikataa Hadiyth zote zisizokuwa na uthibiti wa aya kutoka kwenye Qur-aan.

 

3.       Kosa la kutofautiana lililokuja juu, al-Ijmaa’ haikuwa tena yenye kuwezekana katika kipindi hichi. Kimsingi, hii ni kwa sababu kila kundi lilikosa imani ya wanazuoni wa kila kundi jengine, na hawatokubaliana na maoni yao tena, ama wakikubali au walikataa nao. Kwa kuongezea, Fuqahaa miongoni mwa Swahaabah wameanza kutawanyika sehemu zote za dunia ya Kiislamu, hivyo ilikuwa haiwezekani kwao kukutana kwa lengo la kujadili masuala.

 

4.       Pia katika dunia hii, mapokezi ya Hadiyth na Sunnah zimekuja kuwa maarufu, ambapo kesi hii huko nyuma haikuwahi kuwa kama hivi.

 

5.       Uwongo uliobuniwa wa Hadiyth, kwa sababu nyingi za kutambulika ambazo hatuhitaji kuzijadili hapa zilianza kuenea sana. Kwa mnasaba huu, Waislamu walipokea kwamba Ibn Abbaas alisema: “Tulikuwa tukipokea Hadiyth nyingi kutoka kwa (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) bila ya watu kuwa na woga na ubunifu. Lakini pale watu walipoanza kuwa wazembe katika kusimulia sifa za Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam), tulisimamisha kusimulia Hadiyth.”



[1] Mfano wa Hadiyth zinaitwa mapokezi ya mtu mmoja “Khabar al Waahid” au, kwa wingi, Aahaad. Suala la nafasi ya Hadiyth kama hiyo unajadilwa baadaye kwenye andiko hili.

Share