Skip navigation.
Home kabah

Mema Yaliyobakia الْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ Ni Bora Kuliko Mali Na Watoto

   

15 Shawwaal 1428

 Anasema Allaah سبحانه وتعالى

 

((الْمَالُ وَالْبَنُونَ زِينَةُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ خَيْرٌ عِندَ رَبِّكَ ثَوَابًا وَخَيْرٌ أَمَلاً))

 ((Mali na wana ni pambo la maisha ya dunia. Na mema yanayobakia ni bora mbele ya Mola wako Mlezi kwa malipo, na bora kwa matumaini)) [Al-Kahf: 46]

 

Allaah Ametutajia mapambo ya dunia katika Aaayah hii tukufu, lakini baada ya Kuyataja hayo mapambo Katukumbusha kuwa  mema yanayobakia - َالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ ni bora zaidi kuliko mali na wana. 

 

Ndugu Muislamu jiulize basi: 

 

1-Kwa nini mapambo hayo sio bora kuliko mema yanayobakia?       الْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ  

2-Nini maana yake  mema yanayobakia?َالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ     

 

 Bila ya shaka sote tunayapenda mapambo hayo ya dunia. Na sio hayo tu bali mengi zaidi ya hayo kama Alivyoyataja Allaah سبحانه وتعالى katika aya hii nyingine:

 

 (( زُيِّنَ لِلنَّاسِ حُبُّ الشَّهَوَاتِ مِنَ النِّسَاء وَالْبَنِينَ وَالْقَنَاطِيرِ الْمُقَنطَرَةِ مِنَ الذَّهَبِ وَالْفِضَّةِ وَالْخَيْلِ الْمُسَوَّمَةِ وَالأَنْعَامِ وَالْحَرْثِ ذَلِكَ مَتَاعُ الْحَيَاةِ الدُّنْيَا وَاللّهُ عِندَهُ حُسْنُ الْمَآبِ))  

((Watu wamepambiwa kupenda matamanio ya wanawake, na wana, na mirundi ya dhahabu na fedha, na farasi asili, na mifugo, na mashamba. Hayo ni starehe ya maisha ya duniani; na kwa Allaah ndio kwenye marejeo mema)) [Al-'Imraan: 14]

 

Hata hivyo baada ya kutaja mapambo hayo mengine, Ameendelea Allaah سبحانه وتعالى kutukumbusha tena kwa kutuuliza swali!

((قُلْ أَؤُنَبِّئُكُم بِخَيْرٍ مِّن ذَلِكُمْ لِلَّذِينَ اتَّقَوْا عِندَ رَبِّهِمْ جَنَّاتٌ تَجْرِي مِن تَحْتِهَا الأَنْهَارُ خَالِدِينَ فِيهَا وَأَزْوَاجٌ مُّطَهَّرَةٌ وَرِضْوَانٌ مِّنَ اللّهِ وَاللّهُ بَصِيرٌ بِالْعِبَاد))

((Sema: Nikwambieni yaliyo bora kuliko hayo? Kwa wachamngu ziko Bustani kwa Mola wao zipitazo mito kati yake. Watadumu humo, na wake waliotakaswa, na wanazo radhi za Allaah. Na Allaah ni Mwenye kuwaona waja Wake)) [Al-'Imraan: 15]

 

Kama tunavyoona kuwa yaliyo bora zaidi ya mapambo ya dunia ni Pepo ya Milele na zaidi baada ya kupata Pepo ni kupata Radhi Yake Allaah سبحانه وتعالى.

 

Vile vile kuna hatari yake hayo mapambo kwani huenda wakati mwengine yakawa ni mtihani au adui yetu kama Alivyosema katika aya hizi:

 

 

 ((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا إِنَّ مِنْ أَزْوَاجِكُمْ وَأَوْلَادِكُمْ عَدُوًّا لَّكُمْ فَاحْذَرُوهُمْ))

 

((Enyi mlioamini! Hakika miongoni mwa wake zenu na watoto wenu wamo maadui zenu. Basi tahadharini nao)) [At-Taghaabun: 14]

 

((إِنَّمَا أَمْوَالُكُمْ وَأَوْلَادُكُمْ فِتْنَةٌ وَاللَّهُ عِندَهُ أَجْرٌ عَظِيمٌ))

((Hakika mali yenu na watoto wenu ni jaribio. Na kwa Allaah upo ujira mkubwa)) [At-Taghaabun: 15]

 

Huenda mapambo hayo yakawa adui yetu au majaribio kwani yakasababisha tukayapenda sana hadi yakatupeleka kufanya yasiyomridhisha Allaah سبحانه وتعالى , au yakatughafilisha na kumkumbuka Allaah سبحانه وتعالى , na yakatusahaulisha kabisa na Akhera hadi mauti yatakapotufikia, na mwishowe tukawa ni wenye khasara kubwa kama Alivyosema Allaah سبحانه وتعالى

 

((يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُلْهِكُمْ أَمْوَالُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّهِ وَمَن يَفْعَلْ ذَلِكَ فَأُوْلَئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ))

 

((Enyi mlioamini! Yasikusahaulisheni mali yenu, wala watoto wenu, kumkumbuka Allaah. Na wenye kufanya hayo ndio wenye khasara))  [Al-Munaafiquun: 9]

 

Ama  mema yanayobakia - الْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ haya ndio yatakayotupatia faida kwani hutangulia mapema kuwekwa Akhera yakawa kama hazina ambazo tutazikuta tutakaposimama mbele ya Mola Mtukufu kuhesabiwa siku ya Qiyaamah.

 

Ibn 'Abbaas,  amesema kwamba  mema yanayobakia - َالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ ni kusema:

 

سُبْحَانَ اللهِ،  الحَمْدُ لله ِ,   لاَ إِلَهَ إلاَّ الله ُ, اللهُ أَكْبَر,  لاَ حَوٍلَ وَلا قُوَّةَ إِلاَّ بالله ,  تبَارَكَ اللَّه, أَسْتَغْفِرُ اللَّه

 

Subhana-Allaah, ِAlhamduli-LLaah, Laa Ilaaha Illa Allaah, Allaahu Akbar, Laa Hawlah Wa Laa Quwwata Illa BiLLaah, Tabaraaka Allaah, Astaghfiru-LLaah.

 

 

Vile vile kumswalia Mtume صلى الله عليه وآله وسلم, Swalah tano za kila siku, Hajj, Swaum, Zakaat, Sadaqah, Kuachia huru watumwa, Jihaad, kuungana na ndugu na Jamaa, na vitendo vyote vyema.

 

 عن ثوبان رضي الله عنه قال : قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : ((بخ ٍ بخٍ لخمس ما أثقلهن في الميزان : لا إله إلا الله ، وسبحان الله ، والحمد لله ، والله أكبر، والولد الصالح يتوفى للمرء المسلم فيحتسبه)) النسائي وابن حبان والحاكم ، وأحمد ، وصححه الألباني في صحيح الجامع    

 

Imetoka kwa Thuubaan رضي الله عنه ambaye amesema: Mtume صلى الله عليه وآله وسلم amesema: ((Heko heko kwa vitu vitano, uzito gani vitakavyokuwa  katika Mizani; Laa Ilaah Illa- Allaah,  Wa-Allaahu Akbar, Wa Subhaanah-Allaah, Wa-AlhamduliLLah, na mtoto mwema atakayekufa na wazazi wake wanatarajia thawabu kutoka kwa Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala)) [An-Nasaaiy, Ibn Hibbaan, Al-Haakim, Ahmad, na kaisahihisha Al-Albaaniy katika 'Sahiyh Al-Jaami'i]

 

Kwa hiyo tambua ndugu Muislamu kuwa maskini asiyemiliki nyumba wala mali yoyote wala kitu chochote, lakini amechuma mema yanayobakia - َالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ  japo kutaja hizo tasbiyh pekee ni bora mbele ya Allaah kuliko tajiri mwenye kumiliki mali nyingi lakini hana mema yanayobakia -َالْبَاقِيَاتُ الصَّالِحَاتُ

 

Hii ni miongoni mwa Neema na Rahma za Mola Muumba na Uadilifu Wake kwa waja Zake.