Maonyo Ya Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Kujiepusha Na Kughafilika Kwa Nafsi
Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) Ametuonya tusije kufikia hali ya nafsi kujuta kwa kutokana na kushughulika na mambo ya dunia ambayo ndio sababu kubwa ya kujikuta mtu yuko kwenye 'ghaflah' (kughafilika na Akhera), kusahau kama mauti yako tayari kwa yule iliyomfikia ajali yake bila ya kujua lini au wapi ameandikiwa,
(( وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ مَّاذَا تَكْسِبُ غَدًا وَمَا تَدْرِي نَفْسٌ بِأَيِّ أَرْضٍ تَمُوتُ إِنَّ اللَّهَ عَلِيمٌ خَبِيرٌ))
((Na haijui nafsi yoyote itachuma nini kesho. Wala nafsi yoyote haijui itafia nchi gani. Hakika Allaah Ndiye Mwenye kujua, Mwenye khabari)) Luqmaan:34
Kwa hiyo inapomfikia mtu ajali yake na roho inapotoka hapo nafsi tena hutambua kuwa yale yaliyokuwa yakimshughulisha duniani hayana tena faida naye wala hayawezi kumsaidia wakati huu, ndipo hubaki kujuta na kutambua kuwa yupo katika hasara kubwa!
Tunaona jinsi gani Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) anavyotoa onyo au tanabahisho kwa mwanaadam kwa kughafilika na dhikr (ukumbusho) wa Allaah, na kuendekeza dunia na mapambo yake.
(( يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا لَا تُلْهِكُمْ أَمْوَالُكُمْ وَلَا أَوْلَادُكُمْ عَن ذِكْرِ اللَّهِ وَمَن يَفْعَلْ ذَلِكَ فَأُوْلَئِكَ هُمُ الْخَاسِرُونَ))
((Enyi mlioamini! Yasikusahaulisheni
Bali mwanaadam ni mwingi wa kusahau na kughafilika, pamoja na maonyo na tanbihi zote hizo za Mola wake lakini dunia imemzamisha na kuyanywa maji yake yaliyomlewesha na hadi kutojitambua, mwisho wake ni majuto yale yale ya kutamani kurudishwa duniani afanye mema:
(( وَأَنفِقُوا مِن مَّا رَزَقْنَاكُم مِّن قَبْلِ أَن يَأْتِيَ أَحَدَكُمُ الْمَوْتُ فَيَقُولَ رَبِّ لَوْلَا أَخَّرْتَنِي إِلَى أَجَلٍ قَرِيبٍ فَأَصَّدَّقَ وَأَكُن مِّنَ الصَّالِحِينَ))
((Na toeni katika tulichokupeni kabla hayajamfikia mmoja wenu mauti, tena hapo akasema: Mola wangu Mlezi! Huniakhirishi muda kidogo nipate kutoa sadaka, na niwe katika watu wema)) [Al-Munaafiquun: 10]
Lakini wapi!
(( وَلَن يُؤَخِّرَ اللَّهُ نَفْسًا إِذَا جَاء أَجَلُهَا وَاللَّهُ خَبِيرٌ بِمَا تَعْمَلُونَ ((
(( Wala Allaah Hataiakhirisha nafsi yoyote inapofika ajali yake; na Allaah Anazo khabari za mnayo yatenda)) [Al-Munaafiquun: 11]
Na vilevile Kama Anavyosema Allaah (Subhaanahu wa Ta'ala) tena katika Suratul-Muuminuun:
(( حَتَّى إِذَا جَاء أَحَدَهُمُ الْمَوْتُ قَالَ رَبِّ ارْجِعُونِ))
((Mpaka yanapomfikia mmoja wao mauti, husema: Mola wangu Mlezi! Nirudishe))
(( لَعَلِّي أَعْمَلُ صَالِحًا فِيمَا تَرَكْتُ كَلَّا إِنَّهَا كَلِمَةٌ هُوَ قَائِلُهَا وَمِن وَرَائِهِم بَرْزَخٌ إِلَى يَوْمِ يُبْعَثُونَ))
((
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha



Tunaomba mtuekee section ya
Tunaomba mtuekee section ya kusikiliza adhana.MFANO:-
SHEIKH MISHARY B.RASHID AFASY
tunaomba kisa cha yule
tunaomba kisa cha yule mnafiki aliyezusha alikuwa anashushiwa qur-an zama za MTUME(S.W.A).KUTOKA KWA SH.BACHU