Skip navigation.
Home kabah

Utukufu Wa Ijumaa


27 Rabiy'ul Awwal 1426
 06-05-2005

 

Allaah سبحانه وتعالى   Anasema  

((ذَلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ حُرُمَاتِ اللَّهِ فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ عِندَ رَبِّهِ))  

{Na anaye vitukuza vitakatifu vya Mwenyezi Mungu basi hayo ndiyo kheri yake mbele ya Mola wake Mlezi}Hajj : 22:30

((ذَلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى الْقُلُوبِ))

{Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Mwenyezi Mungu, basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo} Hajj 22:32

Siku ya Ijumaa ni siku tukufu  yetu  waislamu na pia ni siku   aliyoumbwa Adam  عليه السلام na kuingia na kutoka peponi, vile vile ni siku   ambayo Qiyama kitasimama    kama katika hadithi ifuatayo:

 

في الصحيحين عن أبي هريرة رضي الله عنه إن النبي صلي الله عليه وسلم قال عن يوم الجمعة: ( فيه خلق آدم وفيه أدخل الجنة و فيه أخرج منها ولا تقوم الساعة إلا يوم الجمعة)

 

 Kutoka kwa Abi Huraira رضي الله عنه kuwa : Kasema Mtume صلي الله عليه وسلم  kuhusu siku ya Ijumaa {Siku hiyo kaumbwa Adam  na siku hiyo kaingizwa peponi na katolewa, na Qiyaama hakitosimama ila siku ya Ijumaa} Bukhari na Muslim

 

Kwa hiyo tumeichagua siku hii kuwa ni siku ya kupeana nasiha katika ukumbi huu wenu wa Alhidaaya.  Tutajitahidi tuwe tunaweka kila Ijumaa nasiha fupi mpya ili tukumbushane mema  na kukatazana mabaya kama tulivyoamrishwa na Mola wetu  عزوجل .

 

  *******