Utukufu Wa Ijumaa
27 Rabiy'ul Awwal 1426 06-05-2005
Allaah سبحانه وتعالى Anasema
((ذَلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ حُرُمَاتِ اللَّهِ فَهُوَ خَيْرٌ لَّهُ عِندَ رَبِّهِ))
{Na anaye vitukuza vitakatifu vya Mwenyezi Mungu basi hayo ndiyo kheri yake mbele ya Mola wake Mlezi}. Hajj :
((ذَلِكَ وَمَن يُعَظِّمْ شَعَائِرَ اللَّهِ فَإِنَّهَا مِن تَقْوَى الْقُلُوبِ))
{Ndio hivyo! Na anayetukuza ibada za Mwenyezi Mungu, basi hayo ni katika unyenyekevu wa nyoyo} Hajj
Siku ya Ijumaa ni siku tukufu yetu waislamu na pia ni siku aliyoumbwa Adam عليه السلام na kuingia na kutoka peponi, vile vile ni siku ambayo Qiyama kitasimama
في الصحيحين عن أبي هريرة رضي الله عنه إن النبي صلي الله عليه وسلم قال عن يوم الجمعة: ( فيه خلق آدم وفيه أدخل الجنة و فيه أخرج منها ولا تقوم الساعة إلا يوم الجمعة)
Kutoka kwa Abi Huraira رضي الله عنه kuwa : Kasema Mtume صلي الله عليه وسلم kuhusu siku ya Ijumaa {Siku hiyo kaumbwa Adam na siku hiyo kaingizwa peponi na katolewa, na Qiyaama hakitosimama ila siku ya Ijumaa} Bukhari na Muslim
Kwa hiyo tumeichagua siku hii kuwa ni siku ya kupeana nasiha katika ukumbi huu wenu wa Alhidaaya. Tutajitahidi tuwe tunaweka kila Ijumaa nasiha fupi mpya ili tukumbushane mema na kukatazana mabaya
*******
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


