Wanawake Kufuata Jeneza Na Kumswalia Maiti

 

Wanawake Kufuata Jeneza Na Kumswalia Maiti

 

Alhidaaya.com

 

 

Swali:

 

Je inafaa kwa mwanamke kufuatia jeneze hadi misikiti na kumswaliya maiti? Jazaakumullahu kheiran

 

 

Jibu:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Inachukiza kwa wanawake kufuata jeneza kwa kauli ya Ummu 'Atwiyyah (Radhwiya Allaahu 'anhaa) kuwa tulikatazwa kufuata jeneza na haikufanywa ni Shariy’ah kwetu sisi [Muslim].

 

Kumswalia maiti mwanamke anaruhusiwa naye kujiunga katika Swaalah ya Janaazah.

Ingia katika kiungo kifuatacho upate maelezo zaidi  muhimu yanayohusu mas-ala haya:

 

Wanawake Wanayopasa Kufanya Wakati Wa Jeneza Linapotoka

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

 

Share