Masuala Kumi Yanayoeleweka Vibaya Katika Uislam - 5
Chuo Kikuu Cha California Ya Kusini
USC-MSA Muhtasari Ya Maandiko Ya Waislamu
Imefasiriwa na: ‘Abdun-Naaswir Hikmany
Suala Nambari 5 Linaloeleweka Vibaya
Uislamu unamkataa Yesu kwa sababu:
· Yesu hakubaliki kuwa ni ‘mtoto wa Mungu’
JIBU:
Zote mbili; Qur-aan na Sunnah zinatufundisha kwa msisitizo na bila ya wasiwasi kwamba Muumba Anatambua tamko la Utatu kuwa ni uongo ulio mkubwa mno. Qur-aan inaeleza (iliyotafsiriwa)
{{Na (makafiri) husema: “(Mwenyezi Mungu) Mwingi wa rehema amejifanyia mtoto. Bila shaka mumeleta jambo lichukizalo kabisa (kwa kusema hivyo). Zinakaribia mbingu kutatuka kwa (tamko)
Hata hivyo, suala hilo linaloeleweka vibaya haliendani na hoja zinazotolewa hapo juu kwamba Yesu (‘Iysaa) anakataliwa (moja kwa moja). Ni vyema kutanabahisha kwa kusema kwamba inakataliwa kumueleza Yesu (‘Iysaa) kama ni ‘mtoto wa Mungu’. Kwa kuwa ni Mtume wa Allaah, Yesu anatunukiwa cheo chake cha heshima namna walivyopewa Mitume wote, kama ambavyo Aayah ifuatayo inavyotamka (tafsiri):
{{Semeni nyinyi (Waislamu waambiwe Mayahudi na Manaswara; waambieni): “Tumemwamini Mwenyezi Mungu na yale tuliyoteremshiwa, na yale yaliyoteremshwa kwa Ibraahiym na Ismaa’iyl na Is-haaq na Ya’aquub na kizazi (chake Ya’aquub); na waliyopewa Muusa na ‘Iysaa na pia yale waliyopewa Manabii (wengine) kutoka kwa Mola wao; hatutafautishi baina ya yoyote katika hao. (Wote tunawaamini); na sisi tumenyenyekea Kwake.}} [2:136]
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


