028-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kisomo Chake (صلى الله عليه وآله وسلم) Katika Swalah Ya Ijumaa - Sifa Ya Swalah Ya Mtume

 

8-   SWALAH YA IJUMAA

 

 

Alikuwa  (صلى الله عليه وآله وسلم)akisoma mara nyingine katika Rakaa ya mwanzo Suratul-Jumu'aa [62: 11]:

 

 يُسَبِّحُ لِلَّـهِ مَا فِي السَّمَاوَاتِ وَمَا فِي الْأَرْضِ الْمَلِكِ الْقُدُّوسِ الْعَزِيزِ الْحَكِيمِ﴿١﴾

((Vilivyomo katika mbingu na vilivyomo katika ardhi vinamtukuza Allaah, Mfalme, Mtakatifu, Mwenye nguvu, Mwenye hikmah)),

na katika Rakaa ya pili:

 

إِذَا جَاءكَ الْمُنَافِقُونَ

((Wanapokujia wanaafiki)) [63: 11]([1]),

 

na mara nyingine - badala yake([2])- alikuwa akisoma:

 

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ

((Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?)) [88: 26],

na mara nyingine akisoma:

 

سَبِّحِ اسْمَ رَبِّكَ الْأَعْلَى

((Litakase Jina la Mola wako Aliye juu kabisa)) [Al-A'laa 87: 19], katika Rakaa ya mwanzo na:

 

 

هَلْ أَتَاكَ حَدِيثُ الْغَاشِيَةِ

((Je! Imekufikia khabari ya msiba wa kufudikiza?)) [88: 26],

katika Rakaa ya pili([3]).

 

 

[1] Muslim na Abu Daawuud. Imetolewa katika Al-Irwaa (345).

[2] Kifungu kile kile kilichotajwa hapo mbeleni.

[3] Muslim na Abu Daawuud.

Share