Skip navigation.
Home kabah

Bajia Za Dengu Na Viazi

 

Vipimo

 

Unga wa dengu                                       3 vikombe vikubwa

 

Chumvi                                                 1 kijiko cha chai

 

Mbatata (kiazi)                                        1

 

Maji baridi                                             1 glass

 

Baking powder                                        1 cha chai

 

Kotmiri  iliyokatwakatwa                         4 -5 Miche

 

Kitunguu maji kilosagwa                          2 kijiko cha supu

 

Thomu ilosagwa au ya unga                     1 kijiko cha chai

 

Mafuta                                                     500 ml

 

 

 

Namna  Ya  Kutayarisha Na Kupika

 

 

  1. Tumia bakuli  lenye nafasi  mimina unga  na  viungo vyote.

 

 

  1. Tia maji ukitumia uma au mchapo wa mkono (usotumia umeme) kuvuruga mchanganyo.

 

 

  1. Ukisha kuwa laini bila mavimbo, hakikisha si mzito na si uji sana (mwembamba).

 

 

  1. Menya kiazi na kwaruza kiwe mithili ya tambi kisha tia ndani ya unga vuruga uchanganyike.

 

 

  1. Uwache kwa muda wa robo saa (dakika 15) paka 20.

 

 

  1. Weka karai  jikoni au sufuria nzito ndogo, tia mafuta na acha yapate moto sawasawa.

 

 

  1. Tumia kijiko cha supu kuteka unga  kutia kwenye mafuta , unapotia hakikisha kipimo chako chote kimelenga mahala au sehemu moja bila ya kutapakaza ili uweze kupata  kidonge .

 

 

  1. Utaenedelea hivi kwa kujaza karai nafasi yote zikigeuka rangi ya kuiva, unazigeuza upande wa pili paka umalize zikiwiva kwa rangi nzuri.

 

 

  1. Tumia sahani ukiwa umetandaza karatasi za jikoni kuweza kuchuja mafuta baada ya  kuchoma. Kisha badilisha kwenye sahani au bakuli nyengine, tayari kuliwa.

 

 

 

Kidokezo;

 

Huliwa kwa chatini ya aina yoyote, na unapochoma ukiona unga haupandi juu basi lazima kuna itilafu.

 

 

 

assalam aleykum unga wa

assalam aleykum unga wa dengu unaitwaje kwa english

Wa 'alaykumus-salaam wa

Wa 'alaykumus-salaam wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh.

Unga wa dengu unaitwa kwa Kiingereza 'Gram Flour'

Kula kwa siha na afya.