Hadiyth Ya Kumkosoa Kiongozi
SWALI
Je, ipo hadithi inayosema ukitaka kumkosoa kiongozi muone faragha usimkosoe mbele ya ummah?
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allaah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhiya Allaahu ‘anhum) na watangu wema mpaka Siku ya Mwisho.
Shukrani zetu za dhati kwa swali lako kuhusu kumkosoa Kiongozi.
Kutoka kwa Tamiym bin Aws Ad-Daariy (Radhiya Allaahu ‘anhu): Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema: “Dini ni nasiha/nasaha. Tukauliza: Kwa nani? Akasema kwa Allaah, Kitabu Chake, na Mtume Wake, na kwa Viongozi wa Waislamu, na watu wa kawaida. [Muslim]
Na Hadiyth nyingine kuhusu nasaha kwa viongozi, Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) anasema:
“Hakika Allaah Anaridhia kwenu mambo matatu na Anachukizwa nanyi kwa mambo matatu. Anaridhia kwenu kumuabudu Yeye na Kutomshirikisha Yeye na chochote, na kushikamana kwenu na kamba (Dini) ya Allaah bila kufarakana, na kuwanasihi kwenu viongozi wenu wale ambao Allaah Amewapa madaraka juu yenu (viongozi wenu)…” [Ahmad, Maalik na Ibn Hibbaan].
Hakika ni kuwa suala hili linaingia katika mas-ala ya muamala baina ya kiongozi na raia. Wanazuoni wamegawanya mas-ala ya kumkosoa yeyote sio kiongozi tu katika vipengele viwili:
1.
2. Fedheha.
Katika mas-ala ya nasaha inatakiwa ifanywe katika njia nzuri
Viongozi walikuwa wakikosolewa tu mbele ya watu inapokuwa yeye mwenyewe ameomba watu watoe maoni
Hivyo, katika kutoa nasaha inaweza kutegemea na mazingira yenyewe lakini mara nyingi inatakiwa itolewe kwa njia ya faragha.
Na nasaha kwa viongozi wa Kiislam kunaingia: kuwasaidia wao wanapofuata yale ya haki, kuwatii wao katika yale ya sawa, kuwakumbusha wanapokosea au wanaposahau, kuwa na subira juu yao pale wanapofanya mambo ambayo hayapendezi au hayakubaliki, kushirikiana nao katika Jihaad na kutowaasi au kuwafanyia njama katika uongozi wao. Halikadhalika mtu anapaswa awaombee du’aa wawe katika uongofu na ucha Mungu, kwani uongofu wao na ucha Mungu utawanufaisha Waislam wote kwa ujumla.
Ama ushahidi uliotaka wa kumpa Kiongozi nasaha kwa siri ni huu:
Amesema (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam):
“Anayetaka kumpa nasaha Kiongozi kuhusu jambo lolote, basi asimpe nasaha hiyo hadharani, bali amvute mkono pembeni faragha (azungumze naye), na akipokea nasaha hiyo kutoka kwake atakuwa amepata (ni kheri), na akikataa ushauri (nasaha), basi mtu huyo (mwenye kutoa nasaha) atakuwa ashatekeleza wajibu wake.” [Ahmad na Al-Haakim, na Imaam Al-Albaaniy kasema isnaad yake ni Swahiyh].
Na kuna mifano kadhaa ya wema waliopita kuhusiana na utoaji wa nasaha kwa siri, mmojawapo ni ule ulioelezwa na Ibn Rajab kuwa Sa’iyd bin Jubayr alimuuliza Ibn ‘Abbaas (Radhiya Allaahu ‘anhuma), “Je, ninaweza kumuamrisha Kiongozi wangu kufanya ya sawa.” Akamjibu, “Ukiwa una khofu ukimwambia hayo atakuua, basi nyamaza na usiseme chochote kibaya kuhusu Kiongozi huyo. Na ikiwa unashikilia lazima umnasihi, basi ifanye nasaha hiyo baina yako na yeye pekee.” [Ibn Rajab, Kitabu ‘Jaami’I, mj. 1, uk. 225]
Na Allaah Anajua zaidi
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


