Mwanaume Kutoboa Sikio Swalah Zake Zinakubaliwa?

 

Mwanaume Kutoboa Sikio Swalah Zake Zinakubaliwa?

 

Alhidaaya.com

 

 

Swali:

 

Kijana wakiume ametoboa sikio na anasali vipi ibada yake?

 

 

Jibu:

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aalaa) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

 

Kujieguza maumbile kwa kujifananisha na jinsia nyingine ni hila za Shaytwaan ambazo ameahidi kuwapoteza waja na Allaah (Subhaanahu wa Ta'aalaa) Ametuonya naye:

 

إِن يَدْعُونَ مِن دُونِهِ إِلَّا إِنَاثًا وَإِن يَدْعُونَ إِلَّا شَيْطَانًا مَّرِيدًا ﴿١١٧﴾لَّعَنَهُ اللَّـهُ ۘ وَقَالَ لَأَتَّخِذَنَّ مِنْ عِبَادِكَ نَصِيبًا مَّفْرُوضًا ﴿١١٨﴾وَلَأُضِلَّنَّهُمْ وَلَأُمَنِّيَنَّهُمْ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُبَتِّكُنَّ آذَانَ الْأَنْعَامِ وَلَآمُرَنَّهُمْ فَلَيُغَيِّرُنَّ خَلْقَ اللَّـهِ ۚ وَمَن يَتَّخِذِ الشَّيْطَانَ وَلِيًّا مِّن دُونِ اللَّـهِ فَقَدْ خَسِرَ خُسْرَانًا مُّبِينًا ﴿١١٩﴾يَعِدُهُمْ وَيُمَنِّيهِمْ ۖ وَمَا يَعِدُهُمُ الشَّيْطَانُ إِلَّا غُرُورًا ﴿١٢٠﴾أُولَـٰئِكَ مَأْوَاهُمْ جَهَنَّمُ وَلَا يَجِدُونَ عَنْهَا مَحِيصًا ﴿١٢١﴾

Hawaombi badala Yake isipokuwa miungu ya kike na hawaombi isipokuwa shaytwaan muasi. Allaah Amemlaani. Na (shaytwaan) akasema: Kwa hakika nitashika katika waja Wako sehemu maalumu. Na hakika nitawapoteza, na nitawashawishi matamanio ya kulaghai, na nitawaamrisha. Basi watakata masikio ya wanyama (wawatukuze), na nitawaamrisha watabadili maumbile ya Allaah. Na atakayemfanya shaytwaan kuwa rafiki mwandani badala ya Allaah basi kwa yakini amekhasirika khasara bayana.  Anawaahidi na anawashawishi matamanio ya uongo. Na shaytwaan hawaahidi isipokuwa ulaghai. Hao makaazi yao ni Jahannam, na wala hawatopata makimbilio ya kutoka humo.  [An-Nisaa: 117 - 121]

 

 

Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) ametupasha habari kuwa Allaah Amemlaani mwanamme mwenye kujifananisha na mwanamke na kinyume chake.

 

 

Hata hivyo, Ibadah yake ya Swaalah ni sahihi na makosa yake ya kutoboa sikio atapata. Na ni madhambi kama haya ambayo yatamfanya Muislamu siku ya Qiyaama awe ni mwenye kuhasirika na kuwa aliyefilisika kama alivyotuarifu Nabiy (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam). Kwa hiyo, ni vyema sana kwako uweze kuzungumza na kijana huyo na kumuelimisha kuhusu hilo kosa ili aweze kufanya toba na kurudi kwa Allaah Aliyetukuka.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share