034-Sifa Ya Swalah Ya Mtume (Swalla Allaahu 'Alayhi Wa Aalihi Wa Sallam): Kuirefusha Rukuu Na Kukatazwa Kusoma Qur-aan Katika Rukuu

 

KUIREFUSHA RUKUU

 

Alikuwa   (صلى الله عليه وآله وسلم) akifanya rukuu yake, kisimamo chake baada ya rukuu, na sujuud yake na kikao baina sajda mbili, karibu sawa kwa urefu.([1])

 

 

 

KUKATAZWA KUSOMA QUR-AAN KATIKA RUKUU

 

Alikuwa (صلى الله عليه وآله وسلم)  akikataza kusoma Qur-aan katika rukuu na sujuud.([2])

 

Alikuwa akisema: ((Hakika mimi nimekatazwa kusoma Qur-aan hali ya kuwa nimerukuu au nimesujudu. Hivyo basi katika rukuu mtukuzeni Mola (عزوجل), na (ama) katika sujuud, jitahidini kwa du'aa, kwani ni karibu kukubaliwa humo)).([3])

 

 





[1] Al-Bukhaariy na Muslim. Imetolewa katika Irwaa Al-Ghaliyl (331).      

[2] Muslim na Abu 'Awaanah. Makatazo ni ya ujumla, hivyo inahusisha Swalah za Faradhi na Sunnah. Ziada ya Ibn 'Asaakir (17/299/1): "Ama Swalah za Sunnah, hakuna ubaya", ni (aidha) shaadhah au munkar. Ibn 'Asaakir ameashiria dosari humo, hivyo haijuzu kufanyiwa kazi.

[3] Kifungu kile kile kilichotajwa hapo mbeleni.

Share