Shari’ah Inasemaje Kuhusu Mke Kuzikwa Bila Mume Aliye Safarini Kujulishwa

 

Shari’ah Inasemaje Kuhusu Mke Kuzikwa Bila Mume Aliye Safarini Kujulishwa

 

Alhidaaya.com

 

Swali:

 

Mm niliwahi kufunga ndoa na mtoto wa Baba yangu mdogo, faida ya ndoa hiyo nilipata watoto 3, kutokana na maisha nilianza kusafili mpaka leo hii, kwa bahati mbaya mungu alipanga kumchukua kiiumbe chake yani ni mke wangu, baada ya kufaliki malehemu alizikwa bila kufahamishwa mm mume wa mke. Je shelia inasemaje kwa swala hili.

 

 

Jibu: 

 

AlhamduliLLaah - Himidi Anastahiki Allaah (Subhaanahu wa Ta’aala) Rabb wa walimwengu, Swalaah na salamu zimshukie Nabiy Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) na Swahaba zake (Radhwiya Allaahu 'anhum) na waliowafuata kwa wema mpaka Siku ya Mwisho.

 

Inafaa mume ajulishwe pindi mkewe anapoaga dunia ikiwa yuko mbali au karibu. Na vile vile mke anafaa ajulishwe pindi mumewe anapofariki.

 

Kutojulishwa huko kwaweza kuwa kunatokana na kusahamu kwa sababu ya mshtuko kwa kuondokewa na kipenzi chao au hawakuwa na mawasiliano nawe kwa kuwa ulikuwa safari. Inabidi tuwe na dhana nzuri baina yetu. Ama kule kuzikwa kwa mkeo kutakuwa ni sawa kwani Muislamu anapoaga dunia anafaa azikwe haraka asiwe ni mwenye kucheleweshwa.

 

Ni nasaha zetu kwako uwasamehe hao waliokosa kukuarifu kwa kuwapatia udhuru.

 

 

Na Allaah Anajua zaidi

 

 

Share