Wamefariki Kabla Ya Kupewa Mirathi
SWALI:
Swali lenyewe ni
Swali la pili.baba kafariki na ameacha watoto wawili. na wajukuu wawili.baada tuu na watoto wake wawili hawo wakafariki kabla hawajapewa mirathi yao.je;wajukuu hawo wawili wanayo haki ya kumrithi babu yao?nazani swali zangu zimefahamika.na ntashukuru ntapo pata majibu yake.na mungu awaafikishe. Amin.
JIBU:
Sifa zote njema Anastahiki Allah Aliyetukuka Mola Mlezi wa walimwengu wote, Swalah na salamu zimshukie kipenzi chetu Mtume Muhammad (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) ahli zake, Swahaba zake (Radhiya Allaahu 'anhum) na watangu wema mpaka siku ya mwisho.
Japokuwa swali lenyewe lina utata kwani muulizaji hakubaini jinsia ya watoto wa marehemu. Ikiwa hao waliotajwa ndio warithi wa pekee wa marehemu basi wirathi wake utagawanya
1) Hapa mke wa marehemu atapata thumuni (1/8).
2) Ikiwa watoto wote ni wa kiume watagawa wirathi sawasawa baina
3) Ikiwa watoto wote ni wasichana basi watapata thuluthi mbili (2/3) na kila mmoja atapata kiwango sawa cha mirathi.
4) Ikiwa mtoto mmoja ni wa kiume na mwengine ni wa kike,
Ikiwa mke wa marehemu naye alifariki kabla ya kupata sehemu yake katika wirathi basi sehemu yake hiyo itachang’anywa na
Jibu kwa Swali la Pili: Wajukuu kawaida hawamrithi babu
Tanbihi: Ieleweke kuwa wirathi unatolewa tu baada ya:
a) Kulipwa madeni ya marehemu.
b) Kutoa fungu ambalo ameusia marehemu kabla ya kuaga dunia kwake na kisheria halifai kuzidi thuluthi (1/3).
c) Kutoa masrufu ya mazishi kwa mfano sanda, kaburi na mengineyo.
Tanbihi kwa wenye kuuliza Maswali ya Mirathi:
1. Kijana mwanamume.
2. Kijana mwanaume wa kijana mwanaume (mjukuu).
3. Baba.
4. Babu wa kwa baba.
5. Ndugu mume wa kwa baba na mama (khalisa).
6. Ndugu wa kwa baba.
7. Ndugu mume wa kwa mama.
8. Kijana mwanaume wa ndugu mume khalisa.
9. Kijana mwanaume wa ndugu mume wa kwa baba.
10. Ami wa kwa baba na mama.
11. Ami wa kwa baba.
12. Kijana mwanaume wa ami wa kwa baba na mama.
13. Kijana mwanaume wa ami wa kwa baba.
14. Mume.
15. Binti.
16. Binti wa kijana mwanaume.
17. Mama.
18. Dada khalisa.
19. Dada wa kwa baba.
20. Dada wa kwa mama.
21. Bibi mzaa baba.
22. Bibi mzaa mama.
23. Mke.
Hii itatusaidia sana katika kujibu maswali yenu ya mirathi. Shukran.
Na Allah Anajua zaidi.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


