Ndizi Mbichi Kwa Nyama Ya Ng’ombe-2

Ndizi Mbichi Kwa Nyama Ya Ng'ombe - 2

 

Vipimo

Ndizi mbichi  -  10-12

Nyama ng’ombe  - 1 kilo moja

Kitunguu maji - 2

Nyanya/tungule - 2

Kitunguu saumu(thomu/galic) -  7

Tangawizi mbichi  - 1 kipande

Ndimu  - 2 kamua

Chumvi -   kiasi

Mafuta -    3 vijiko vya supu

Tui la nazi - 3 vikombe

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika

  1. Saga kitunguu thomu na tangawiz mbichi.
  2. Weka nyama katika sufuria tia kijiko kimoja cha kitunguu thomu na tangawizi, chumvi na ndimu  kisha chemsha hadi iive.
  3. Menya ndizi ukatekate
  4. Weka mafuta katika sufuria tia kitunguu maji kilokatwakatwa ukaange kidogo tu kisha tia nyanya/tungule uendelea kukaanga.
  5. Tia tangawizi na thomu ilobakia.
  6. Tia ndizi, kaanga kidogo kisha tia supu ya nyama na nyama yake.
  7. Ziache ndizi ziive zikiwa tayari tia tui la nazi zikiwa tayari.

 

 

Share