054 - Al-Qamar
الْقَمَر
Al-Qamar: 054
بِسْمِ اللَّـهِ الرَّحْمَـٰنِ الرَّحِيمِ
اقْتَرَبَتِ السَّاعَةُ وَانشَقَّ الْقَمَرُ ﴿١﴾
1.
Saa imekaribia na mwezi umepasuka.
وَإِن يَرَوْا آيَةً يُعْرِضُوا وَيَقُولُوا سِحْرٌ مُّسْتَمِرٌّ ﴿٢﴾
2. Na wanapoona dalili hukengeuka na husema: Sihiri ya siku zote, tumeizoea.
وَكَذَّبُوا وَاتَّبَعُوا أَهْوَاءَهُمْ ۚ وَكُلُّ أَمْرٍ مُّسْتَقِرٌّ ﴿٣﴾
3. Na wakakadhibisha (haki), na wakafuata hawaa zao, na kila jambo litafikia ukomo.
وَلَقَدْ جَاءَهُم مِّنَ الْأَنبَاءِ مَا فِيهِ مُزْدَجَرٌ ﴿٤﴾
4. Na kwa yakini imekwishawajia kati ya habari muhimu ambayo ndani yake kuna makemeo makali.
حِكْمَةٌ بَالِغَةٌ ۖ فَمَا تُغْنِ النُّذُرُ ﴿٥﴾
5. Ni hikmah iliyofikia upeo timilifu kabisa lakini hayafai kitu maonyo.
فَتَوَلَّ عَنْهُمْ ۘ يَوْمَ يَدْعُ الدَّاعِ إِلَىٰ شَيْءٍ نُّكُرٍ ﴿٦﴾
6. Basi jitenge nao (ee Muhammad صلى الله عليه وآله وسلم). Siku atakayoita muitaji kuliendea jambo baya mno la kuogofya.
خُشَّعًا أَبْصَارُهُمْ يَخْرُجُونَ مِنَ الْأَجْدَاثِ كَأَنَّهُمْ جَرَادٌ مُّنتَشِرٌ ﴿٧﴾
7. Macho yao yakiwa dhalili, watatoka katika makaburi kama kwamba wao ni nzige waliosambaa.
مُّهْطِعِينَ إِلَى الدَّاعِ ۖ يَقُولُ الْكَافِرُونَ هَـٰذَا يَوْمٌ عَسِرٌ ﴿٨﴾
8. Wakikimbia mbio kwenda kwa muitaji huku wamebenua shingo zao. Makafiri watasema: Hii ni siku ngumu mno!
كَذَّبَتْ قَبْلَهُمْ قَوْمُ نُوحٍ فَكَذَّبُوا عَبْدَنَا وَقَالُوا مَجْنُونٌ وَازْدُجِرَ ﴿٩﴾
9. Walikadhibisha kabla yao kaumu ya Nuwh, wakamkadhibisha Mja Wetu, wakasema: Majnuni. Na akakaripiwa.
فَدَعَا رَبَّهُ أَنِّي مَغْلُوبٌ فَانتَصِرْ ﴿١٠﴾
10. Basi akamwita Rabb wake: Hakika mimi nimeshindwa nguvu basi Nusuru.
فَفَتَحْنَا أَبْوَابَ السَّمَاءِ بِمَاءٍ مُّنْهَمِرٍ ﴿١١﴾
11. Tukafungua milango ya mbingu kwa maji yanayofoka na kumiminika kwa nguvu.
وَفَجَّرْنَا الْأَرْضَ عُيُونًا فَالْتَقَى الْمَاءُ عَلَىٰ أَمْرٍ قَدْ قُدِرَ ﴿١٢﴾
12. Na Tukazibubujua ardhi chemchemu, basi yakakutana maji kwa amri iliyokwisha kadiriwa.
وَحَمَلْنَاهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلْوَاحٍ وَدُسُرٍ ﴿١٣﴾
13. Na Tukambeba kwenye ile (jahazi) yenye mbao na misumari.
تَجْرِي بِأَعْيُنِنَا جَزَاءً لِّمَن كَانَ كُفِرَ ﴿١٤﴾
14. Inatembea chini ya Macho Yetu, ni jazaa kwa yule aliyekuwa amekanushwa.
وَلَقَد تَّرَكْنَاهَا آيَةً فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ ﴿١٥﴾
15. Na kwa yakini Tumeiacha iwe ni mazingatio. Je basi yuko yeyote mwenye kuwaidhika?
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ ﴿١٦﴾
16. Basi vipi ilikuwa Adhabu Yangu na Maonyo Yangu?
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ ﴿١٧﴾
17. Na kwa yakini Tumeiwepesisha Qur-aan ili ipate kusomwa, kuhifadhiwa na kufahamika. Basi je, yuko yeyote mwenye kuwaidhika?
كَذَّبَتْ عَادٌ فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ ﴿١٨﴾
18. Kina ‘Aad walikadhibisha. Basi vipi ilikuwa Adhabu Yangu na Maonyo Yangu?
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ رِيحًا صَرْصَرًا فِي يَوْمِ نَحْسٍ مُّسْتَمِرٍّ ﴿١٩﴾
19. Hakika Sisi Tuliwapelekea upepo wa adhabu; wa sauti kali na baridi kali katika siku ya nuhsi yenye kuendelea mfululizo.
تَنزِعُ النَّاسَ كَأَنَّهُمْ أَعْجَازُ نَخْلٍ مُّنقَعِرٍ ﴿٢٠﴾
20. Unawang’oa watu kama kwamba ni vigogo vya mtende vilong’olewa.
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ ﴿٢١﴾
21. Basi vipi ilikuwa Adhabu Yangu na Maonyo Yangu?
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ ﴿٢٢﴾
22. Na kwa yakini Tumeiwepesisha Qur-aan ili ipate kusomwa, kuhifadhiwa na kufahamika. Basi je, yuko yeyote mwenye kuwaidhika?
كَذَّبَتْ ثَمُودُ بِالنُّذُرِ ﴿٢٣﴾
23. Kina Thamuwd walikadhibisha maonyo.
فَقَالُوا أَبَشَرًا مِّنَّا وَاحِدًا نَّتَّبِعُهُ إِنَّا إِذًا لَّفِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ ﴿٢٤﴾
24. Wakasema: Ah! Tumfuate binaadamu mmoja miongoni mwetu? Hakika hapo sisi tutakuwa katika upotofu na wazimu.
أَأُلْقِيَ الذِّكْرُ عَلَيْهِ مِن بَيْنِنَا بَلْ هُوَ كَذَّابٌ أَشِرٌ ﴿٢٥﴾
25. Ah! Ameteremshiwa yeye tu ukumbusho baina yetu? Bali yeye ni muongo mkubwa, mfidhuli mwenye kutakabari mno.
سَيَعْلَمُونَ غَدًا مَّنِ الْكَذَّابُ الْأَشِرُ ﴿٢٦﴾
26. Watakuja kujua kesho nani muongo mkubwa mfidhuli mwenye kutakabari mno.
إِنَّا مُرْسِلُو النَّاقَةِ فِتْنَةً لَّهُمْ فَارْتَقِبْهُمْ وَاصْطَبِرْ ﴿٢٧﴾
27. Hakika Sisi Tutawapelekea ngamia jike awe jaribio kwao. Basi (ee Nabiy Swaalih عليه السلام) watazame na vuta subira.
وَنَبِّئْهُمْ أَنَّ الْمَاءَ قِسْمَةٌ بَيْنَهُمْ ۖ كُلُّ شِرْبٍ مُّحْتَضَرٌ ﴿٢٨﴾
28. Na wajulishe kwamba maji ni mgawanyo baina yao (ngamia na wao), kila sehemu ya maji itahudhuriwa (kwa zamu).
فَنَادَوْا صَاحِبَهُمْ فَتَعَاطَىٰ فَعَقَرَ ﴿٢٩﴾
29. Wakamwita swahibu wao, akakamata (upanga) akaua (ngamia).
فَكَيْفَ كَانَ عَذَابِي وَنُذُرِ ﴿٣٠﴾
30. Basi vipi ilikuwa Adhabu Yangu na Maonyo Yangu?
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ صَيْحَةً وَاحِدَةً فَكَانُوا كَهَشِيمِ الْمُحْتَظِرِ ﴿٣١﴾
31. Hakika Sisi Tuliwapelekea ukelele angamizi mmoja tu, basi wakawa kama mabuwa makavu ya mtengenezaji zizi.
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ ﴿٣٢﴾
32. Na kwa yakini Tumeiwepesisha Qur-aan ili ipate kusomwa, kuhifadhiwa na kufahamika. Basi je, yuko yeyote mwenye kuwaidhika?
كَذَّبَتْ قَوْمُ لُوطٍ بِالنُّذُرِ ﴿٣٣﴾
33. Kaumu ya Luutw walikadhibisha maonyo.
إِنَّا أَرْسَلْنَا عَلَيْهِمْ حَاصِبًا إِلَّا آلَ لُوطٍ ۖ نَّجَّيْنَاهُم بِسَحَرٍ ﴿٣٤﴾
34. Hakika Sisi Tuliwapelekea tufani ya mawe isipokuwa familia ya Luutw. Tuliwaokoa nyakati kabla ya Alfajiri.
نِّعْمَةً مِّنْ عِندِنَا ۚ كَذَٰلِكَ نَجْزِي مَن شَكَرَ ﴿٣٥﴾
35. Neema kutoka Kwetu. Hivyo ndivyo Tunavyomlipa ambaye ameshukuru.
وَلَقَدْ أَنذَرَهُم بَطْشَتَنَا فَتَمَارَوْا بِالنُّذُرِ ﴿٣٦﴾
36. Na kwa yakini aliwatahadharisha Nguvu Zetu za kuadhibu lakini wakatilia shaka maonyo.
وَلَقَدْ رَاوَدُوهُ عَن ضَيْفِهِ فَطَمَسْنَا أَعْيُنَهُمْ فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ ﴿٣٧﴾
37. Na kwa yakini walimshawishi awape wageni wake, Nasi Tukawapofoa macho yao. Basi onjeni Adhabu Yangu na Maonyo Yangu.
وَلَقَدْ صَبَّحَهُم بُكْرَةً عَذَابٌ مُّسْتَقِرٌّ ﴿٣٨﴾
38. Na kwa yakini iliwafikia asubuhi mapema adhabu ya kuendelea.
فَذُوقُوا عَذَابِي وَنُذُرِ ﴿٣٩﴾
39. Basi onjeni Adhabu Yangu na Maonyo Yangu.
وَلَقَدْ يَسَّرْنَا الْقُرْآنَ لِلذِّكْرِ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ ﴿٤٠﴾
40. Na kwa yakini Tumeiwepesisha Qur-aan ili ipate kusomwa, kuhifadhiwa na kufahamika. Basi je, yuko yeyote mwenye kuwaidhika?
وَلَقَدْ جَاءَ آلَ فِرْعَوْنَ النُّذُرُ ﴿٤١﴾
41. Na kwa yakini watu wa Firawni walifikiwa na maonyo mengi.
كَذَّبُوا بِآيَاتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذْنَاهُمْ أَخْذَ عَزِيزٍ مُّقْتَدِرٍ ﴿٤٢﴾
42. Walikadhibisha Ishara Zetu zote, Tukawakamata mkamato wa Mwenye Enzi na Nguvu Asiyeshindika, Mwenye Uwezo wa juu kabisa.
أَكُفَّارُكُمْ خَيْرٌ مِّنْ أُولَـٰئِكُمْ أَمْ لَكُم بَرَاءَةٌ فِي الزُّبُرِ ﴿٤٣﴾
43. Je, makafiri wenu (enyi Maquraysh) ni bora kuliko hao (ummah) wa awali? Au mna msamaha katika Maandiko Matukufu?
أَمْ يَقُولُونَ نَحْنُ جَمِيعٌ مُّنتَصِرٌ ﴿٤٤﴾
44. Au wanasema: Sisi ni wengi tutashinda tu.
سَيُهْزَمُ الْجَمْعُ وَيُوَلُّونَ الدُّبُرَ ﴿٤٥﴾
45. Utashindwa mjumuiko wao na watageuka nyuma (watimue mbio).
بَلِ السَّاعَةُ مَوْعِدُهُمْ وَالسَّاعَةُ أَدْهَىٰ وَأَمَرُّ ﴿٤٦﴾
46. Bali Saa ndio miadi yao, na Saa ni janga kubwa na chungu zaidi.
إِنَّ الْمُجْرِمِينَ فِي ضَلَالٍ وَسُعُرٍ ﴿٤٧﴾
47. Hakika wahalifu wamo katika upotofu na wazimu.
يَوْمَ يُسْحَبُونَ فِي النَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمْ ذُوقُوا مَسَّ سَقَرَ ﴿٤٨﴾
48. Siku watakayoburutwa motoni kifudifudi: Onjeni mguso wa moto mkali mno.
إِنَّا كُلَّ شَيْءٍ خَلَقْنَاهُ بِقَدَرٍ ﴿٤٩﴾
49. Hakika Sisi Tumekiumba kila kitu kwa Qadar (makadirio, majaaliwa).
وَمَا أَمْرُنَا إِلَّا وَاحِدَةٌ كَلَمْحٍ بِالْبَصَرِ ﴿٥٠﴾
50. Na Amri Yetu haiwi ila ni moja tu, kama upepeso wa jicho.
وَلَقَدْ أَهْلَكْنَا أَشْيَاعَكُمْ فَهَلْ مِن مُّدَّكِرٍ ﴿٥١﴾
51. Na kwa yakini Tumewaangamiza wenzenu. Je, basi yuko yeyote mwenye kuwaidhika?
وَكُلُّ شَيْءٍ فَعَلُوهُ فِي الزُّبُرِ ﴿٥٢﴾
52. Na kila kitu wakifanyacho kimo katika madaftari ya rekodi.
وَكُلُّ صَغِيرٍ وَكَبِيرٍ مُّسْتَطَرٌ ﴿٥٣﴾
53. Na kila kidogo na kikubwa kimeandikwa.
إِنَّ الْمُتَّقِينَ فِي جَنَّاتٍ وَنَهَرٍ ﴿٥٤﴾
54. Hakika wenye taqwa watakuwa katika Jannaat na mito.
فِي مَقْعَدِ صِدْقٍ عِندَ مَلِيكٍ مُّقْتَدِرٍ ﴿٥٥﴾
55. Katika makao ya haki kwa Mfalme Mwenye Nguvu zote, Mwenye Uwezo wa juu kabisa.
