Imaam Al-Albaaniy: Asiolewe Mwanamke Hadi Aache Kufanya Kazi

 

Asiolewe Mwanamke Mpaka Aache Kufanya Kazi

 

Imaam Al-Albaaniy (Rahimahu Allaah)

 

Alhidaaya.com

 

 
Aliulizwa Imaam Al-Albaaniy (Rahimahu Allaah):

 

"Je, mwenye kuposa anaweza kumuomba mwanamke ambaye anataka kumposa kuacha kufanya kazi?"

 

Akajibu:
"Mwenye kuposa hana jukumu hilo juu yake. Hata hivyo, asimuoe ikiwa kama anafanya kazi nje ya nyumba (yake). Haijuzu kwako kumposa na kumuoa ikiwa anafanya kazi nje ya nyumbani kwake."

 

[Silsilat Al-Hudaa Wa An-Nuwr, kanda namba 174]

 

 

 

Share