Skip navigation.
Home kabah

Nini Hukumu Ya Nywele Za Bandia?

 

 

SWALI

Asalaam aleykum,

Naomba kufahamishwa zaidi juu ya nywele za bandia.Siku hizi zipo nyuzi za sweta ambazo hutumika kusukia nywele, hizi si nywele wala si nywele za bandia lakini hufanya nywele zikaonekana ndefu je vipi hukumu yake?

 

 


JIBU:

BismiLLaah wa AlhamduliLLaah was-Swalaatu wa Salaamu ‘alaa Muhammad wa ‘alaa  aalihi wa Aswhaabihil Kiraam, wa ba’ad:

Kubandika nywele za bandia ni katika maovu aliyotuhadharisha Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  kwamba Allaah سبحانه وتعالى  Humlaani mwanamke anayefanya hivyo kama ilivyo katika Hadiyth ifuatayo:

Mwanamke wa Ki-Answaari aliyemuozesha binti yake ambaye nywele zake zilianza kung'ooka.  Mwanamke huyo wa Ki-Answaari alikuja kwa Mtume صلى الله عليه وآله وسلم  na kumtajia kwamba "Mumewe (mume wa mwanangu) ameona kwamba nimwachie avae nywele za bandia" Mtume صلى الله عليه وآله وسلم akasema, ((Usifanye hivyo kwani Allaah سبحانه وتعالىHuteremsha laana Yake kwa wanawake kama hao wanaoongeza nywele za bandia))   [Al-Bukhariy 7:133  kutoka kwa Bibi 'Aishah ]  

Makatazo katika Hadiyth hiyo yamekuja kwa ujumla kuharamishwa kuvaa  nywele  za bandia au kuunga nywele    kwa hiyo hata kama zinazotumika sio nywele hasa bali ni nyuzi au chochote kingine, hukumu inabakia ni hiyo hiyo nayo ni kuharamishwa kufanya hivyo na adhabu yake ni kupata laana kutoka kwa 'Allaah سبحانه وتعالى . Na laana ni kuwa mbali na rahma za Allaah سبحانه وتعالى .

Bila ya shaka hakuna atakaye kupata laana ya Allaah سبحانه وتعالى  kwa hiyo dada zetu wajaribu kujiepusha na maovu kama haya  na waridhike na maumbile Aliyowajaalia Mola wao.

Na Allah Anajua zaidi.

 

asalam aleykum Naomba

asalam aleykum Naomba kufahamishwa mwanamke akitoa nyusi vipi hukumu yake.