Uji Wa Sembe

Uji Wa Sembe

 

 

Vipimo   

 

Unga wa sembe (fine corn flour) vijiko 5 vya kulia mjazo

Maziwa ½ kikombe

Maji vikombe 2 ½ takriban

Pilipili manga ½ kijiko cha chai

Sukari upendavyo

chumvi ukipenda chembe

 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika 

  1. Changanya unga wa sembe katika kibakuli pamoja na maji kiasi ukoroge.
  2. Weka maji yaliyobakia katika sufuri kisha mimina unga uliokoroga, uchemshe huku unakoroga dakika chache.
  3. Tia maziwa, sukari pilipili manga ukiwa tayari.  

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)  

 

 

Share