Skip navigation.
Home kabah

Shurba



 

VIPIMO

 

 Nyama ya mbuzi ya mafupa au ya ng'ombe       Kilo moja

Mafuta                                                                   2 vijiko vya supu

Vitunguu maji (vikate vidogo vidogo)                2

Nyanya (kata ndogo ndogo)                               1

Thomu na tangawizi iliyosagwa                         2 vijiko vya supu

Bizari ya pilau ya unga (Jeera)                          1 kijijo cha chai

Gilgilani ya unga (Dania)                                   ½  kijiko cha chai

Pilipili manga ya unga                                       1 kijiko cha chai

Mdalasini wa unga                                              ¼ kijiko cha chai

Kotmiri (iliyokatwa ndogo ndogo)                     kiasi

Nanaa (iliyokatwa ndogo ndogo)                      kiasi

Chumvi                                                               kiasi

Siki                                                                     3 vijiko vya supu  

Ngano (Oats) au *ngano nzima                         2 vikombe

* ikiwa ngano nzima basi roweka kwa  muda wa masaa na uchemshe mpaka  

   ziwive.

NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA

  1.      Chemsha nyama na chumvi kwa maji kiasi  mpaka iwive

2.      Katika sufuria nyengine, weka mafuta na kaanga vitunguu kidogo tu vilainike, usiviwache kugeuka rangi.

3.      Weka bizari zote, pili pili manga, chumvi.

4.      Tia thomu na tangawizi.

5.      Tia nyanya na bila ya kuzikaanga sana tia nyama na supu yake.

6.      Tia kotmiri, nanaa.

7.      Pembeni changanya ngano (oats) na maji koroga kisha tia katika supu ya shurba.

8.      Iwache ichemke kidogo tu ngano ziwive.

9.      Tia siki na tayari kuliwa. 

Shukrani kwa mapishi bora

Shukrani kwa mapishi bora lakini nina swali mbili tafadhali nieleze kotmiri ni nini?
Tafadhali nieleze naana ni nini?

Wa 'alaykumus-salaam wa

Wa 'alaykumus-salaam wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh

Tunashukuru kwa maoni yako.

Kotmini ni corriander na naanaa ni mint leaves.

Ndugu Zako
AL HIDAAYA