Shurba
(1).jpg)
VIPIMO
Nyama ya mbuzi ya mafupa au ya ng'ombe Kilo moja
Mafuta 2 vijiko vya supu
Vitunguu maji (vikate vidogo vidogo) 2
Nyanya (kata ndogo ndogo) 1
Thomu na tangawizi iliyosagwa 2 vijiko vya supu
Bizari ya pilau ya unga (Jeera) 1 kijijo cha chai
Gilgilani ya unga (Dania) ½ kijiko cha chai
Pilipili manga ya unga 1 kijiko cha chai
Mdalasini wa unga ¼ kijiko cha chai
Kotmiri (iliyokatwa ndogo ndogo) kiasi
Nanaa (iliyokatwa ndogo ndogo) kiasi
Chumvi kiasi
Siki 3 vijiko vya supu
Ngano (Oats) au *ngano nzima 2 vikombe
* ikiwa ngano nzima basi roweka kwa muda wa masaa na uchemshe mpaka
ziwive.
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1. Chemsha nyama na chumvi kwa maji kiasi mpaka iwive
2. Katika sufuria nyengine, weka mafuta na kaanga vitunguu kidogo tu vilainike, usiviwache kugeuka rangi.
3. Weka bizari zote, pili pili manga, chumvi.
4. Tia thomu na tangawizi.
5. Tia nyanya na bila ya kuzikaanga
6. Tia kotmiri, nanaa.
7. Pembeni changanya ngano (oats) na maji koroga kisha tia katika supu ya shurba.
8. Iwache ichemke kidogo tu ngano ziwive.
9. Tia siki na tayari kuliwa.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha



Shukrani kwa mapishi bora
Shukrani kwa mapishi bora lakini nina swali mbili tafadhali nieleze kotmiri ni nini?
Tafadhali nieleze naana ni nini?
Wa 'alaykumus-salaam wa
Wa 'alaykumus-salaam wa RahmatuLLaahi wa Barakaatuh
Tunashukuru kwa maoni yako.
Kotmini ni corriander na naanaa ni mint leaves.
Ndugu Zako
AL HIDAAYA