Pai Ya Kuku (Chicken Pie)

VIPIMO
Unga wa kitobosha (puff pastry) 397-400 gm
Nyama ya kuku bila ya mifupa ratili (LB)
Kabichi iliyokatwa nyembamba
nyembamba 2 Vikombe vya chai
Thomu/Tangawizi iliyosagwa 1 kijiko cha chakula
Chumvi kiasi
Pili pili manga 1 kijiko cha chakula
Jirah (bizari ya pilau) 1 kijiko cha chai
Mdalasini 1 kijiko cha chai
Dania (corriander powder) 1 kijiko cha chai
Ndimu au limau 2 Vijiko vya chakula
NAMNA YA KUTAYARISHA NA KUPIKA
1.
2. Washa jiko la oveni moto wa kiasi cha kiwango 375-400 Deg.
3. Kata nyama ya kuku vipande vipande kisha itie kwenye sufuria na tia ndani yake, thomu/tangawazi, chumvi, pilipili manga, jirah, mdalasini dania na ndimu.
4. Mpike kuku kwa moto mdogo mdogo hadi awive. Akihitaji maji, tia kidogo tu kiasi cha kumpika awive asibakie na maji.
5. Epua na chambua kuku. (Unaweze kutumia sehemu ya kuku ya mifupa, hivyo itabidi uchambue na kutoa mifupa pembeni).
6. Sukuma unga wa kitobosha (puff-pastry). (Ukipenda kata madonge mawili zitokee pai mbili).
7. Kuku atakuwa ameshapoa, mchanganye na kabichi vizuri ongeza vikolezo ukipenda kama chumvi, pilipili manga na ndimu.
8. Weka mchanganyiko wa kuku na kabichi katikakati katika unga uliosukuma na kata kama miba ya samaki (
9. Suka kufunika vizuri kuku, huku unabana msuko ili ugandane.

11. Pika katika oven ambalo litakuwa tayari limeshashika moto unaohitajika. Pika hadi zigeuke rangi na ziwive.
12. Epua, ziweke katika sahani ya kupakulia zikiwa tayari.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


