Fatwaair Za Jibini Kwa Kunyunyizia Ufuta Na Habbat Sawdaa

 Fatwaair Za Jibini Kwa Kunyunyizia Ufuta Na Habbat Sawdaa

Vipimo 

Unga - 3 vikombe

Hamira - 1 kijiko cha kulia

Baking powder -  ½ kijiko cha chai

Maziwa ya unga - ½ kikombe

Maji dafudafu (warm) - 1 kikombe

Mafuta au siagi -  1/3 kikombe

Sukari - 2 vijiko vya kulia

Yai - 1

Chumvi -   ½ kijiko cha chai

Jibini (cheese) ya kukatakata - kiasi

Ufuta na habbah sawdaa (haba soda)-  kiasi

Yai la kupakazia 

Namna Ya Kutayarisha Na Kupika  

  1. Changanya unga, hamira, maziwa, sukari, baking powder, chumvi.
  2. Katika kibakuli, changanya maziwa na maji yadafudafu (warm).
  3. Mimina maziwa katika unga, tia mafuta, na vitu vingine uchanganye vizuri na kukanda kidogo tu.
  4. Acha uumuke kiasi uwe saizi mara mbili yake.
  5. Fanya vidonge kisha sukuma uweke vipande vya jibini (cheese)
  6. Funga vikate kwa design upendavyo.
  7. Panga katika treya uliyopakaza siagi.
  8. Piga yai jengine vizuri kwa uma (fork) upakaze kwa brush kisha nyunyizia ufuta na habbah sawdaa.
  9. Pika (bake) katika moto wa 200 degrees takriban mpaka viwe rangi ya hudhurungi.
  10. Epua vitamu  kwa chai. 

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kufurahika)

 

 

 

 

 

 

Share