Supu Ya Mchanganyiko Wa Adesi Za Nazi Kwa Celery Karoti Viazi Mchicha

Supu Ya Mchanganyiko Wa Adesi Za Nazi Kwa Celery Karoti Viazi Mchicha

 

Vipimo

 

Machanganyiko wa adesi za kijani, nyekundu, brown - vikombe 2

Celery – mche mmoja  

Karoti - 1

Viazi - 2

Bizari njano ½ kijiko

Jira (cumin, bizarii ya pilau) 1 kijiko cha chai

Paprika – 1 kijiko cha chai

Gilgilani (coriander) - 1 kijiko cha chai

Tangawizi mbichi- 2 vijiko vya chai

Nyanya kopo – vijiko 2 vya supu

Tui la nazi – vikombe 2

Mchicha – vikombe 3

Supu yoyote upendayo

Mafuta -  ¼ kikombe

 

 

Namna Ya Kutayarisha Na kupika

 

  1. Weka mafuta katika sufuria tia vitunguu, kaanga kidogo kisha tia celery, karoti na viazi kaanga kidogo.
  2. Tia bizari zote, chumvi, tia maji kidogo.
  3. Tia adesi zote, kisha tia supu ya kutosha koroga.
  4. Tia nyanya kopo kisha acha ipikike viive vitu vyote na kuwa nzito kidogo.
  5. Tia tui la nazi (ukipenda), tia mchicha koroga kidogo tu ili mchicha usipikike sana.
  6. Epua ikiwa tayari.
  7. Unapopakua katika vibakuli tia juu yake mtindi kiasi vijiko viwili, nyunyizia kotmiri, pilipili mbichi zilokatwakatwa (ukipenda) na kitunguu kilokatwakatwa kwa ajili ya kupambia na kuzidisha ladha.

 

Bis-swihhah wal-hanaa (kula kwa siha na kuburudika)

 

 

Share