Vikeki Vidogo Vya Chenga Za Shayiri

Vipimo
Unga 2 Vikombe
Chenga za shayiri (oatmeal) 1Kikombe
Baking Powder 1 Kijiko Cha Supu
Baking Soda ½Kijiko Cha Chai
Chumvi ½Kijiko Cha Chai
Sukari Ya Buni 1 Kikombe
(Brown Sugar)
Mdalasini 1 Kijiko Cha Chai
Kungu manga (nutmeg) ½Kijiko Cha Chai
Mayai 2
Mafuta ½Kikombe
Mtindi (yogurt) 1½ Vikombe
Vanilla 1 Kijiko Cha Chai
Karoti Ziliokunwa(grated) 1 Kikombe(Karoti 3)
Namna Ya Kutayarisha Na Kupika
1. Chunga pamoja unga, oatmeal, baking powder, baking soda, chumvi, sukari ya buni, mdalasini na kungu manga.
2. Changanya mayai, mafuta, mtindi na vanilla kwenye bakuli.Tia karoti kisha ule mchanganyiko wa unga.
3. Chota mchanganyiko kwa kijiko tia ndani ya treya maalum ya kupikia muffins/cupcakes.
4. Pika (bake) katika oveni lenye moto wa 350º F kwa dakika 30.
- Login or register to post comments
- Email this page
- Chapisha


